Stephano Simbeye,
VWAWA:
Naibu Katibu Mkuu wa chama cha Walimu Tanzania (CWT) Ezekiel
Oluoch amelaani kitendo kinachofanywa na baadhi ya walimu cha kuongeza
wanafunzi hewa na kuwa amechukizwa na tabia hiyo ambayo amesema imekifedhehesha
chama hicho na kwamba serikali ichukue hatua kali Zaidi ya kuwavua madaraka.
Kauli hiyo aliitoa jana katika ukumbi wa kanisa la Moravian
Nsala mjini Vwawa wilayani Mbozi mkoani Songwe kuwa tabia baadhi ya walimu
wakuu kuzidisha idadi ya wanafunzi ili wajipatie kipato cha ziada imekikata
mapembe kutokana na kuwa kimekuwa kikipambana kutaka walimu wakuu wa shule za
msingi na wakuu wa shule za sekondari kupatiwa posho na stahiki nyingine
nyingi.
“ jambo hili linanifanya nikose usingizi kutokana na
jitihada tunazofanya kuwapigania walimu harafu tunasikia wanafanya mambo ya
kipuuzi ambayo yamekikata mapembe chama hicho, ambapo hivi sasa walimu wakuu
wameanza kupatiwa posho hizo” alisema Oluoch
Alisema serikali iwachukulie hatua kali, Zaidi ya kuwavua
madaraka walimu hao pia amewakumbusha walimu hao umuhimu wa kutimiza wajibu wao
kuwa upo kwa mujibu wa sheria za mahusiano kazini
Mmoja wa walimu Grace Chanya akizungumzia suala la baadhi ya
walimu wakuu kuongeza idadi ya wanafunzi hewa kuwa inatokana na mfumo mbaya wa
utunzaji takwimu ambapo mwalimu wa darasa anakuwa na takwimu zake kupitia
daftari la mahudhurio, huku mwalimu Mkuu wa shule ana takwimu kupitia daftari
la usajili wa wanafunzi.
Alisema chanzo cha takwimu hizo kupishana ni kutokana na
wanafunzi wanaohamia kutoingizwa kwenye kumbukumbu zote na hivyo kuleta tofauti
inayojitokeza.
Habari Zaidi zinaeleza kuwa mchezo wa kuzidisha wanafunzi
umekuwa ukifanyika muda mrefu tangu kipindi ambacho serikali ilikuwa ikitoa
fedha za ruzuku (capitation glant), na kuwa hali hii inachangiwa na mamlaka
kutokuwa makini katika takwimu.
Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya mbozi Edina
Mwaigomole akizungumza kwa njia ya simu kuhusu tatizi la baadhi ya walimu wakuu
kuzidisha idadi ya wanafinzi kwa lengo la kudanganya ili wapatiwe fedha za
ziada zinazotolewa na serikali katika utekelezaji wa elimu bure, alisema tayari
ameunda kamati ndogo ya uhakiki anbayo anatarajia umpatie ripoti wiki ijayo
ambayo atalinganisha na takwimu zilizopo.
Tayari katika mikoa ya Arusha, simiyu na wilaya ya Kinondini jijini Dar es salaam kuwapo kwa idadi kubwa ya wanafunzi hewa.
Tayari katika mikoa ya Arusha, simiyu na wilaya ya Kinondini jijini Dar es salaam kuwapo kwa idadi kubwa ya wanafunzi hewa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment