Stephano
Simbeye,Mbozi.
Rai hiyo ilitolewa jana na aliyekuwa
mgombea wa urais kupitia chama hicho Edward Lowasa kwa niaba ya umoja wa katiba
ya wananchi UKAWA wakati akizungumza na wanachama wa chama hicho wilayani Mbozi
mkoani Songwe katika ukumbi wa Moravian Vwawa mjini.
Lowasa alisema kuwa maandamano na
migomo ya kiharakati inaweza kusababisha watanzania wakapigana wenyewe kwa
wenyewe na kuwataka wanachama wa chama hicho wavunje makundi yaliyojitokeza
wakati wa uchaguzi na kukijenga chama ili kiweze kushika dola katika uchaguzi
mkuu wa mwaka 2020
Aliitaka serikali kuruhusu mikutano
ya vyama vya siasa ili kila chama kitimize haki yake ya kikatiba ya kufanya
mikutano kuimarisha vyama vyao na si mikutano kuwa ya upande mmoja wa chama
tawala.
Mwenyekiti wa baraza la wazee
wa chama hicho Hasheem Juma Issa akizungumzia kuhusu operasheni UKUTA alisema
kuwa wameamua kufikisha ujumbe kwa wananchi kwa kufanya maandamano ya amani
Septemba Mosi mwaka huu na kuongeza kuwa hilo si la mkoa wa Songwe pekee bali
ni nchi nzima huku maandamano hayo yakiambatana na mikutano ya hadhara.
Aidha aliongeza kuwa kulingana na
katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaruhusu vyama vya Siasa kufanya
mikutano, hivyo na wao waruhusiwe kufanya mikutano hiyo kwa kuwa Tanzania ni ya
watanzania wote na hivyo misingi ya kikatiba iheshimiwe.
Naye kada wa chama hicho ambaye pia
ni Diwani wa kata ya Ichenjezya Bahati Mbughi alisema chama kipeleke ruzuku
katika ngazi za chini ili kusukuma nguvu katika kukijenga huku akiwataka
wanachama wenzake wa CHADEMA kuachana na chuki zinazozalishwa wakati wa kura za
maoni kipindi cha uchaguzi na kuacha kuitana mamluki.
Naye Richard Kibona aliwataka
viongozi wa ngazi za juu kuacha kupokea malalamiko kutoka kwa kila mtu na
kuyafanyia kazi bali watazame nani kayapeleka na jinsi ya kuyatatua si kuchukua
maamuzi bila kutazama msingi wa malalamiko hayo na kuutaka uongozi wa chama
hicho kuunda tume maalum ya kuchunguza makosa hayo.
Aidha mara baada ya mkutano huo
kumalizika msafara wa Lowasa ulilekea Tunduma na hatimaye safari ya kuelekea
Sumbawanga mkoani Rukwa kuendeleza mikakati ya chama hicho.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment