Na Stephano Simbeye,Mbozi
WATUMISHI watano wa halmashauri ya wilaya ya
Mbozi mkoani Songwe ambao wamehamishwa na wengine kustaafu wanatakiwa
kurejeshwa ili kuja kutoa maelezo matumizi ya zaidi ya Sh. 410 milioni
zilizopotea kwa mazingira tata.
Hayo yapo kwenye mapendekezo ya Tume
iliyoundwa na mkuu wa mkoa wa Songwe Luteni Mstaafu Chiku Galawa kuchunguza
upotevu wa fedha hizo katika halmashauri ya wilaya ya Mbozi, kufuatia imeshindwa
kukamilisha uchunguzi wake baada ya kukosa nyaraka muhimu, hivyo kulazimika
kuwaita maofisa waliohusika licha ya kuwa wengine walikwishastaafu ili
kukamilisha uchunguzi wake.
Akisoma sehemu ya taarifa hiyo Mwenyekiti
wa kamati hiyo ya watu wanne Kastory Msigala alisema kamati yake ilipewa hadidu
za rejea tatu ili kuzifanyia kazi ambazo ni pamoja na kujua iwapo fedha
zinazolalamikiwa zilifika katika halmashauri ya Mbozi, kufahamu malengo
mahususi ya fedha hizo na iwapo zilitumika kwa malengo yaliyokusudiwa na ni
miradi gani iliyokusudiwa kutumia fedha hizo.
Alisema katika uchunguzi wake tume
imejiridhisha kuwa fedha hizo ziliingia katika akaunti ya halmahshauri ya Mbozi
kiasi cha Sh. 410,136,002 na kuwa zililetwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo na
mfuko wa barabara kwa mtiririko kuwa, Julai 19, 2012 ziliingizwa Sh.
233,019,897, Agosti 2, 2012 ziliingizwa Sh. 38,774,600 na Oktoba 19, 2011
ziliingizwa Sh. 133,341,585 na kufanya jumla ya Sh. 410,136,002.
Msigala alisema hata hivyo tume hiyo
imeshindwa kupata majibu halisi jinsi fedha hizo zilivyo tumika baada ya kukosa
hati za malipo, hata hivyo kamati hiyo imebaini kuwa Sh. 238 milioni ziliingia
na zikahamishwa kwenda kwenye akaunti mpya ya pamoja ambayo ilikuwa na fedha nyingi
wakati huo ilikuwa na fedha nyingi zaidi ya Sh. 2bilioni hali hiyo pia
ilisababisha kukosa hati za malipo.
Aliendelea kueleza kuwa Sh. 38 milioni
zilihamishiwa kwenye akaunti ya mishahara katika ofisi ya Mganga mkuu ambapo
pia madokezo yaliyohamisha fedha hizo hayakupatikana pi takwimu na kumbukumbu
za watumishi waliolipwa fedha hizo kama mshahara hazikupatikana.
Msigala alisema pia walihitaji kuona miradi
ambayo fedha hizo zilipelekwa lakini hawakupata na kuwa maofisa walioitwa
kwenye tume hiyo ili kutoa maelezo wengi hawakuwepo wakati huo hivyo kuhitaji
maofisa waliokuwepo wakati huo akiwemo Mkurugenzi mtendaji, Mtunza hazina,
Ofisa elimu sekondari Ofisa Mipango na Mganga mkuu wa wilaya ili kupata
maelezo.
Diwani wa kata ya Isasa Emir Mzumbwe akichangia
hoja hiyo alisema suala hilo limeigharimu halmashauri kwa kukosa fedha za
maendeleo kufuatia kupata hati zenye mashaka ambapo awali ilidaiwa kuwa fedha
hizo hazikuingizwa na hivyo kulazimika kutuma watu kufuatilia hazina.
Alisema ni vizuri wahusika wakatafutwa
popote walipo ili waje watoe maelekezo vipi fedha hizo zilitumika.
Sebastian Kilindu ni Diwani wa kata Mlowo
Sebastian alisema pamoja na watumishi hao kuitwa ili wahojiwe pia Mwenyekiti wa
halmashauri Erick Ambakisye anastahili kukaa pembeni ili kupisha uchunguzi kwa
faida y halmashauuri na pia kulinda heshima yake.
Mwanasgheria wa halmashauri ya wilaya ya
Mbozi Deogratus Nchimbi alisema kuna vyombo vinavyohusika kuwaita watumishi hao
ni vizuri vitumike kufuata utaratibu wa kisheria na kwa hatua ambayo suala hili
limefikia ni vizuri vyombo vya dola vifanye kazi yake.
Katibu tawala mkani hapa Elia Ntandu alisema
bada ya tume hiyo kukosa majibu mkuu wa mkoa ameagiza maofisa waliohusika
wakamatwe ikiwemo waliohamishwa na waliostaafu hata hivyo alisema mtumishi
mmoja uhamisho wake umestishwa na tayari yuko wilayani hapa kwa ajili ya hoja
hiyo.
Naye Mwenyekiti wa halmashauri ya Mbozi
Elick Ambakisye akizungumzia tuhma hizo zilizomhusisha nay eye alidai kuwa
tuache taratibu zifuatwe na ukweli utajulikana.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment