Social Icons

Wednesday, 3 May 2017

DC John Palingo AishauriIdara ya Afya



Stephano Simbeye, Mbozi


Idara ya afya ya halmashauri ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, imeshauriwa kuunganisha kampeni zake za kiafya kwa pamoja ili kurahisisha matumizi ya rasilimali chache zilizopo, ili zilete tija.

Ushauri huo umetolewa jana na mkuu wa wilaya ya Mbozi John Palingo wakati alipotembelea moja ya kituo cha chanjo  katika zahanati ya serikali ya Mlowo, kuwa ili jukabiliana na changamoto ya ukosefu wa vitendea kazi kama magari ni vyema kampeni mbalimbali zikafanywa pamoja ili rasilimali hizo chache zitumike vizuri.

"Kampeni mnazofanya kama vile damu salama huduma za tiba kwa mkoba na nyingine nyingi zifanywe kwa pamoja"alisema mkuu huyo wa wilaya.

Kauli hiyo ilifuatiwa na kauli ya mganga mkuu wilayani hapa Dr. Janeth Makoye kueleza changamoto inayokwamisha shyghuli za chanjo kuwa ni pamoja na ukosefu wa vyombo vya usafiri,majokofu na upungufu wa dawa za chanjo hasa uliojitokeza mwaka jana. Alisema wilaya Mbozi ina jumla ya vituo vya kutolea chanjo 62 lakini kati ya hivyo 44 ndivyo vinafanyakazi hivyo kulazimika jutoa huduma kwa kutumia kliniki inayotembea.

Aidha Dr. Makoye akizunfumzia chanjo alisema mwaka jana walifikiwa watoto 16927 kati ya watoto 18808 waliokuwa wamekusudiwa ambayo ni sawa na asilimia 90 na kuwa katika mwaka huo hapakuwepo na taarifa za magonjwa yaliyojitokeza ambayo yanazuilika kwa njia ya chanjo.

Aliongeza kuwa kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu wamewafikia na kuwapatia chanjo watoto 4806 kai ya watoto 4905 sawa na asilimia 98 ya lengo kwa kipindi hicho kwa kuwachanja kwa magonjwa dhidi ya Surua, pepopunda, porio, kifaduro, donda koo, homa ya ini, homa ya uti wa mgongo na kichomi na kuwa kauri mbiu inasema "Jamii iliyochanjwa ni jamii yenye afya bora"

mmoja wa akina mama aliyefika kupatia chanjo mwanae Ezra Njowela alisema kujitokeza kupata chanjo hiyo kunatokana na mafunzo wanayopata tangu uja uzito wanapohudhuria kliniki, hali inayofanya kujua umuhimu wa kuhudhuria kliniki na umuhimu wa chanjo, hivyo kutambua faida za kuwachanja watoto wao na hasara ya kutochanja.
mwisho

No comments:

Post a Comment