Na:
Manuel Kaminyoge- Mbozi
Wamiliki na watumiaji
wa vyombo vya usafili mkoani Songwe na
nchi nzima kwa ujumla wametakiwa kuhakikisha bima zao kama ni halali ili
kuepusha usumbufu unaoweza kutokeza pindi matatizo yanapojitokeza kwa upande wa abilia ama gari lenyewe
kuharibika .-
Kauli hiyo ilitolewa na
Muhasibu wa mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) Nyanda za Juu Kusini Kulenje Mbura kuhusiana
na wamiliki wa magari na madereva, kuwa makini pale wanapokata Bima kwa
mawakala wanao husika na ukataji wa sticker za Bima, ambapo aliwaonya wale wanatoa
sticker feki kuacha mara moja kwani hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Kwa upande wake Meneja wa NIC
LTD Tanzania mkoa wa mbeya Ally Mohamed alipokuwa akizungumza na
wandishi wa habari na kuongeza kuwa wamiliki
wengi wa vyombo vya moto na watumiaji hawana elimu namna ya kujua Bima ya
bandia na halisi hali inayosababisha usumbufu wawapo barabarani.
Mohamed alisema kuwa
baada ya zoezi la ukaguzi wa Bima hizo katika
mkoa wa Songwe wamebaini kuwapo matumizi ya Bima bandia hali
inayosababishwa na watumiaji wengi wa vyombo vya moto kupenda kupitia njia za
mkato
Mmoja wa madereva
Asante Rashidi alilalamikia zoezi hilo kuwa linakabiliwa na changamoto kubwa ya
kukaa kwa muda mrefu wakati wa kukaguliwa wakipoteza muda mwingi bila kufanyakazi hali
inayofanya kukwamisha safari zao na kusababisha kupata hasara kwa kushindwa
kutimiza malengo.
Mwanasheria wa Mamlaka
ya Bima Tanzania Nyanda za Juu Kusini (TIRA)
Michael Mbena alisema kuwa madereva na wamiliki wa vyombo vya moto wanatakiwa
kufika katika ofisi za kutolea Bima ili kuepukana na makanjanja ambao
wamesambaa nchi nzima ,ikiwa ni pamoja na kupata elimu inayo husu masuala ya
bima ya vyombo vya usafiri.
Aliongeza kuwa hatua
kali za kisheria zitachukuliwa kwa wale wote ambao watakiuka sheria na taratibu
za kupata bima ya vyombo vya usafiri.
mwisho
Na: Manuel
Kaminyoge, Mbozi
Wanachi wa wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, wameaswa
kulinda na kutunza mazingira kwa kutofanya shughuli za kilimo katika vyanzo vya
maji kitendo ambacho ni kosa la jinai na ni kinyume cha sheria.
Hayo yalisemwa na Katibu Tawala wilayani hapa Tusubilege
Benjamin ambaye alikua mgeni rasmi
katika sherehe za maadhimisho ya siku ya mazingira duniani, ambazo kiwilaya zimefanyika kata ya Hezya
akimuwakilisha mkuu wa wilaya ya Mbozi John Palingo lengo ikiwa ni kuhamasisha
wananchi kijijini hapo kutunza mazingira kutokana na kata hiyo kukithiri kwa
uharibifu wa mazingira.
Alisema suala la mzingira ni la dunia nzima na
kwamba kufuatia hilo sababu kubwa ya
maadhimisho hayo ni kubuni mikakati mbali mbali itakayosaidia kupunguza
uharibifu wa mazingira, jamii kuwajibika katika kupanda miti kwa ajili ya
matumizi mbali mbali na kutoa elimu ya mazingira katika Nyanja mbalimbali
hususani masuala ya afya na usafi wa mazingira.
Baadhi ya wananchi kijijini hapo walisema sheria ya
mazingira kutaka shuguli za kibinadamu kutofanyika ndani ya mita 60 imewaathiri kwakuwa wengi wao wanategemea kujipatia kipato kwa
kulima kilimo cha umwagiliaji.
Maiko Mkumbo aliiomba
serikali ipunguze mita 60 badala yake waweke mita 30 ili ziwasaidie kujipatia
kipato.
Awali katika risala iliyosomwa na ofisa wa mazingira
wilaya ya Mbozi mkoani hapa Hamis Nzunda alisema wilaya ya Mbozi imefanikiwa kuwa na vyanzo
vingi vya maji pamoja na misitu lakini
kutokana na changamoto za wananchi kuvamia maeoneo hayo kwa kufanya za kilimo katika vyanzo hivyo kitendo ambacho ni kinyume na sheria ya
mazingira na 20 ya mwaka 2004.
Nzuda alisema sheria inatoa hamasa kwa wananchi na
wadau mbali mbali kuendesha shughuli
rafiki katika maeneo hayo kama ufugaji nyuki na bustani za miche ya miti na
mabwawa ya samaki.
Mwisho
Na: Manuel Kaminyoge, Mbozi
Wakazi wa vijiji
vya Chizumbi na Ukwile kata ya Isandula wilayani Mbozi mkoani Songwe, wameanza
kutengeneza kipande cha barabara kwa nguvu yao katika eneo oevu baada ya mkandarasi
anayetengeneza Barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 5 kushindwa kutokana na
eneo hilo kuwa na maji mengi.
Potea Mwembe, alisema makubaliano ya kujitolea ujenga kipande hicho
yalifikiwa mwishoni kwa wiki katika eneo hilo ambapo kufuatia kero wanayoipata
ya kushindwa kupita eneo hilo.
Malaika
Mbisa alisema kuwa wapo tayari kutumia nguvu yao ili ghalama zilizokuwa
zinatakiwa kutumika eneo hilo badala yake zihamishiwe mbele ili kuimarisha
barabara hiyo ambayo itaunganisha na kijiji jilani cha Mbebe wilayani Ileje na
kurahisisha mawasiliano.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Isandula Vasco Msongole aliwapongeza wananchi wake kwa makubaliano
waliyoyaamua na kwamba wameonyesha ushilikiano na moyo wa uchungu juu ya
ukosefu wa barabara katika eneo hilo kwa muda mrefu.
Mwenyekiti wa halimashauri ya Mbozi Elick Ambakisye licha ya
kuwapongeza wananchi hao kwa hatua hiyo pia alisema kuwa anawahakikishia kuwa
pesa yao waliyotengewa kuhusu barabara hiyo itafanya kazi ipasavyo ili kuleta
mawasiliano na muunganiko mzuri wa vijiji hivyo.
Ambakisye aliongeza kuwa atahakikisha anasimamia barabara
hiyo inatengenezwa kwa ustadi na kwamba itasaidia kuleta maendeleo ya kata hiyo
na kurahisisha mawasiliano kwa wananchi wa kijiji cha chizumbi na chimbuya.
Aidha barabara ya Chimbuya – Chizumbi yenye urefu wa kilometa
5 inajengwa na mkandarasi Subiri Ndambo inatarajia kukamilika mwezi ujao.
Mwisho
No comments:
Post a Comment