Mbozi: Mkuu wa mkoa wa Songwe Chiku Galawa
amemjia juu Meneja wakala wa barabara mkoa (Tanroads) kwa kuandaa kikao cha
bodi ya barabara kwa kutumia makaratasi badala ya kutumia teknolojia ya tehama.
Galawa alisema hayo Jana akifungua
kikao hicho ambacho kilifanyika katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi
uliopo katika mji wa Vwawa kuwa hajafurahishwa na kitendo cha mkutano huo
kuandaliwa kwa kutumia makabrasha wakati alipiga marufuku ili kupunguza
matumizi ya fedha za serikari ili zipelekwe katika miradi mingine ya maendeleo.
Alisema anashangaa kuona wajumbe wa
Bodi hiyo wanatumia makabrasha badala ya Tehama wakati wajumbe wengi
walikwishagawiwa (ipad) ambapo makabrasha ya wajumbe yangetumwa kupitia humo na
wajumbe wangekuwa wakitumia teknolojia hiyo kujadiliana.
Mkoa wa Songwe uliazimia kutumia
teknolojia ya mawasiliano (TEHAMA) katika vikao vyake mbalimbali ili
kurahisisha mawasiliano lakini pia kupunguza gharama kubwa iliyokuwa ikitumika
kuandaa makabrasha na kuyafikisha kwa wajumbe katika vikao vya mabaraza ya
madiwani ambapo kwa mwaka zinatumika zaidi ya Sh. 50 milioni.
Meneja wakala wa Barabara mkoani
hapa Yohani Kasaini alisema kuwa alikiri na kusema kwamba hali hiyo haitajirudia
tena kutumia makabrasha katika vikao vijavyo.
ambapo pia alisema mkoa wa songwe kwa sehemu
kubwa kuna changamoto ya miundo mbinu ambapo fedha inayotelewa ni ndogo
ukilinganisha na uhitaji wa mkoa ambapo kwa mwaka 2017na 2018 mkoa wa songwe
umetengewa bilioni 10. 1
mkuu wa wilaya ya momba juma saidi
irando alisema kuwa anawaomba meneja wa TRD mkoan na TARURA wakafanye ukaguzi
wa madaraja mawili yaliyojengwa katika harimashauri ya momba ambayo licha ya kujengwa
hayatumiki na wananchi Huku yakionekana kujengwa chini ya kiwango.
Ubatizo japyon sonsa mwenyekiti wa
harimashauri ya wilaya ya ileje amesema kuwa wakandalasi wengi wamekuwa
wakifanya kazi kwa mazoea ambapo wakati mwingine wanakaa nje na makambi yao na
wakati mwingine kazi inasimama zaidi ya wiki mbili na kuvuka mda wa mkataba
huku wananchi wakipata shida kubwa juu ya mawasiliano ya barabara ambapo pia
alipendekeza barabara ya mpembe, isongole, kwenda kyela inatengenezwa ili
kufungua mawasiliano kati ya wilaya ya kyela na ileje.
Ernest mgeni mratibu wa tarura mkoa
wa songwe alisema kuwa kutokana na uchanga wa mkoa changamoto ni nyingi lakini
atahakikisha anawasimamia vilivyo mameneja waliowekwa kila wilaya ili
kurahisisha huduma kwa wananchi.
Aidha
katika kikao hicho Galawa alisema kuwa wakuu wa wilaya ya Momba Jumaa Irando wanachunguza kwa ukaribu wakandalasi waliopewa
tends katika wilaya husika ili kuakikisha fedha za wananchi zinasimamiwa vizuri
na kuwawajibisha wale watakaofanya kazi kwa mazoea
No comments:
Post a Comment