Stephano Simbeye,
MBOZI: Halmashauri tano za mkoa wa Songwe zimeshindwa
kuchangamkia fursa ya kupata zaidi ya Sh. 800milioni zinazotokana na malipo kwa watoa huduma za afya yanyotolewa na mfuko
wa taifa wa bima ya afya (NHIF) kufuatia kushindwa kuwasajili wazee zaidi ya 40000
ambao wangewezesha kupata fedha zaidi
kwa ajili ya kuboresha huduma ya afya kupitia mpango wa tele kwa tele.
Kitendo hicho kimemkasilisha mkuu wa mkoa wa Songwe Chiku
Galawa ambapo alisema kitendo cha kutotekeleza agizo lake la kuwalipia watu
wenye umri wa zaidi ya miaka 60 badala ya kuwatengenezea vitambulisho vya
msamaha vinavyogharimu Sh 5000 kila kimoja na badala yake wawalipie gharama ya
kujiunga kwenye mfuko wa afya ya jamii (CHF) Sh. 10,000 fedha ambayo
ingerejeshwa kwao mara mbili zaidi na mfuko wa taifa wa bima ya afya hivyo
kuboresha upatikanaji wa dawa na vitendanishi.
“ Naona suala la
kuwalipia wazee ni mgomo kwa kuwa tuliagizana tangu mwaka jana lakini
mlisingizia kuwa hamkuliweka katika bajeti, mwaka huu mumeliweka kwenye bajeti lakini
utekelezaji wake unasua sua tatizo lenu ni ubinafsi ingetokea safari hapa leo
leo fedha zingepatikana mnajiangalia ninyi zaidi kuliko wengine kwa vile ninyi
mkiugua mnapata matibabu” alisema Galawa.
“Mkiwalipia wazee mtarudishiwa fedha zenu kupitia mfuko wa
tele kwa tele marambili na hivyo kuwa chanzo kingine cha mapato ambacho
kitawasaidia kuboresha huduma za afya sijui ni kwanini hamtaki sasa nawaagiza na
hapa sitaki mchezo ifikapo januari wazee wote muwe mumewaingiza kwenye mfuko wa
bima ya afya ya jamii CHF na Bado mtatakiwa kuwalipia watoto na yatima na
wanaoishi katika mazingira magumu. “
alisisitiza mkuu huyo wa mkoa.
Mkuu huyo wa mkoa alizungumza hayo mwishoni mwa wiki
iliyopita wakati wa kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa (RCC) kilichofanyika
mjini Vwawa katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Mbozi.
Wakijibu hoja ya mkuu wa mkoa wakurugenzi wa halmashauri hizo walidai kwamba katika
kipindi kilichopita walikuwa wakifanya kazi ya kuwatambua wazee kwanza ndipo
hatua nyingine za kuwasajili katika mfuko wa afya ya jamii ifuate.
Kaimu Mkurugenzi mtendaji
katika halmashauri ya Mji wa Tunduma Kastroy Msigala alisema tayari
halmashauri yake imewatambua wazee 1154 hatua za kuwalipia zimeanza isipokuwa
bado wazee 151 na kwamba wataongeza
zaidi ili kukamilisha ifikapo Januari.
Mkurugenzi halmashauri ya Momba Adriano Jungu alikiri kuwa
kulikuwa na matatizo ya Takwimu ambapo hadi sasa inaonesha kuna wazee 8000
katika halmashauri yake na kuwa michango iliyotolewea Januari Juni walililpia
zaidi ya watu 50.
Kwa upande wake Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya
(NHIF) mkoani hapa alisema vituo vya afya vya serikali havichangamkii fursa
iliwewekwa na serikali ambapo watoa huduma ya afya wanaowasajili wapata huduma
za afya kupitia mfuko wa bima ya afya ya jamii wanapatiwa fedha nyingine kiasi
kama hicho kwa lengo la kuboresha huduma za afya.
Alisema maelekezo ya fedha zinazorejeshwa kwa watumia huduma
yanataka asilimia 77 ya fedha zinazorejeshwa zitumike kwa ajili ya kununua dawa
na vitandanishi na kiasi kinachobaki kinaweza kutumika kwa matumizi mengine ya
uendeshaji na kwamba halmashauri kutochangamkia hilo ni kupoteza fursa.
Aidha hadi sasa zaidi ya wazee 40402 wamekwishatambuliwa katika halmashauri
zote mkoani hapa ambapo kila mmoja akilipiwa bima ya afya ya jamii kiasi cha
Sh. 10,000 zitapatikana zaidi ya Sh. 404,020,000 ambazo zikitolewa mara dufu
yake zinapatikana zaidi ya Sh. 808,040,000 ambazo zingesaidia kuboresha huduma
za afya.
Mwisho
No comments:
Post a Comment