Social Icons

Friday, 14 October 2016

Bavicha Wataka Serikali Ifungue Mipaka Wananchi Wauze Mazao yao

Na: Stephano Simbeye



VIONGOZI wa Baraza la wanawake la Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) wamekerwa na kitendo cha Serikali kuwazuia wakulima kuuza mazao yao kwenye masoko ya nje ya nchi huku ikishindwa kuwapunguzia bei ya pembejeo za ruzuku,

Viongozi wa baraza hilo,ambao pia ni wabunge ni Risala kabongo,mbunge viti maalum mkoa wa Songwe,Hawa Mwaifunga viti maalum Tabora,Kunti Yusuph viti maalum DododomaNagy Kaboyoka mbunge jimbo la Same mashariki,walitembelea wilaya zote mkoani humo kuzungumza na wanawake wenzao.

Viongozi hao,waliweza kuzungumza na wanawake wenzao mambo mbalimbali pamoja na  changamoto na kero zinazowakabili na kupanga namna ya kupambana nazo ambapo waliahidi kuzipeleka bungeni ili zikafanyiwe kazi.

Susan Simchimba,mkazi wa Mbozi,alisema wilaya hiyo,imekuwa na changamoto nyingi ikiwemo kuuziwa pembejeo kwa bei kubwa ambazo ni feki huku mazao wanayoyapata japo ni kidogo wanapewa masharti namna na mahara pa kuuzia mazao yao.

Asanga Juma mkazi wa Mbozi,alisema changamoto kubwa inayowakabiri ni ukosefu wa fedha asilimia tano zinazotengwa na serikali kwenye halmashauri kwa ajili ya wanawake na vijana licha ya kuwa wameanzisha vikundi lakini wamekuwa hawapati fedha hizo.

Risala Kabongo mbunge viti maalum mkoani Songwe,alisema ni kosa serikali kumpangia mkulima sehemu za kuuza mazao yake wakati amelima kwa shida ili auze mahala atakapo ili aweze kupata fedha za kuendeshea maisha kwa kuwa asilimia 75 wamategemea kilimo.

Alisem atakapo rudi bungeni atazipeleka kero hizo ili zifanyiwe kazi,ikiwa ni pamoja na kuikumbusha serikali kupunguza bei za pembejeo kwa kuwa walilizungumzia bungeni linasubili utekelezaji na kuwa kuhusu asilimia 5 fedha za vijana na wanawake atazungumza na wabunge wenzake ili zitolewe.

Nao wabunge viti maalum Hawa Mwaifunga wa Tabora,Kunti Yusuph wa Dododma na Nagy Kaboyoka mbunge wa Same mashariki,kwa nyakati tofauti,walisema wamezikusanya kero zote zinazowahusu wanawake na kuwa wanaendelea kwenda maeneo mengineyo ili kupata kero na wataziwakirisha bungeni.

Walisema wanawake wa mkoa wa Songwe pamoja na wananchi kwa ujumla wamekuwa wakikabiriwa na changamoto nyingi ambazo zinahitaji usimamizi na ufuatiliaji,hivyo walisema wataungana na mbunge mwenyeji Risala Kabongo kuziondoa changamoto za wananchi.

Baada ya viongozi hao wa Bawacha ambao pia ni wabunge kuzunguka wilaya zote za mkoa wa Songwe baadaye walimsindikiza mbunge mwenyeji ambaye aliitisha mkutano wa adhara jimbo la Mbozi ambapo alizungumza na wananchi na kuchukua kero mbalimbali akiahidi kuzipeleka bungeni.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment