Social Icons

Tuesday, 18 October 2016

Mkuu wa mkoa wa Songwe Akemea Majungu asema yatauchelewesh mkoa kupata Maendeleo



Stephano Simbeye, Mbozi

Mkuu wa mkoa wa Songwe Luteni Mstaafu Chiku Galawa amekemea vilali marumbano yanayoendelea ya kuzusha uongo kuhusu mahali pa kujenga ofisi ya mkoa kuwa yanawachelewesha kufikia malengo ya kujiletea maendeleo ya haraka ya mkoa. 

Kauli hiyo ameitoa leo alipokuwa akizungumza na madiwani katika kikao cha kupitia hoja za mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali (CAG) kuwa kumekuwa na vikao visivyo rasmi ambavyo vimezua ubishani usiokuwa na afya na kudai kuwa mkoa unaiburuza halmashauri ya wilaya kwa kubatilisha uamuzi wa awali wa maeneo yaliyopendekezwa kujengwa ofisi za mkuu wa mkoa.

 " waheshimiwa madiwani tunakoenda siko tutachelewesha maendeleo ya wanasongwe na kuwa taratibu za kufikia hatua ya maamuzi bado haijafikiwa maneno yanatoka wapi nawaasa acheni ubinafsi tufanye kazi kwa manufaa ya mkoa wetu"alihoji Galawa 

Alisema hivi sasa wataalamu wanapitia maeneo mengi ili kubaini fursa zilizopo na baadaye vikao halali vitafanyika na kuwa zitashindanishwa hoja na vigezo na eneo litakalokuwa na vigezo vinavyokubalika litapitishwa kwa utaratibu uliopo na si vinginevyo.

 Alisema kila mmoja ajiulize maswali muhimu ambayo yatasaidia kuupeleka mbele mkoa kimaendeleo kwani maendeleo si jengo la ofisi ya mkuu wa mkoa pia kuna vyuo vya ufundi stadi veta na shughuli nyingine za uwekezaji. " alihoji

“Acheni kugombea ofisi itajengwa wapi acheni wataalamu wabaineshe vizuri fursa za maeneo zilizopo, na tuwe wamoja kuhakikisha tunakwenda salama, mimi niko hapa nimeletwa nifanye kazi nitaondoka na wenye mkoa mtakaobaki mtakuja kumbuka wakati mmekwishakosea na kujutia" alisema mkuu huyo wa mkoa

Akizungumza wakati wa kufunga Mwenyekiti wa halmashauri ya Mbozi Elick Ambakisye alisema chanzo cha migogoro na ubishani huo unatokana na kuwapo baadhi ya viongozi (hakuwataja) wanaofanya vikao na mikutano isiyo rasmi ambayo inajadili suala la makao makuu pasipo kushirikisha wadau wengine.

“ Mheshimiwa Mkuu wa mkoa kuna  viongozi wenzetu wanafanya vikao mbadala ambavyo vimekuwa vikituvuruga muda mrefu wilayani kwetu kwa mfano tunasimamia sheria ya mazingira inyokataza kulima ndani ya mita sitini, lakini kuna viongozi wenzetu wanakwenda kufanya mikutano ya hadhara na kuwaambia watu walime ndani ya mita tano” alisema Ambakisye

Aidha kumekuwa na mijadala miongoni mw wakazi wa Vwawa kufuatia taarifa kwamba serikali inafanya mchakato wa kutafuta eneo linguine la kujenga makao makuu ya mkoa nje ya maeneo matatu yaliypendekezwa.
Mwisho

No comments:

Post a Comment