Social Icons

Friday, 14 October 2016

Wakazi wa Vwawa Wataka Mbunge Aeleze sababu za kuwapo Hati za Mashaka




VWAWA:Baadhi ya wakazi wa Jimbo la Vwawa wilayani Mbozi mkoani Songwe,jana walimtaka mbunge wa jimbo hilo, Japhet Hasunga (CCM) kuwapa majibu ya sababu wilaya ya Mbozi kupata hati yenye mashaka kwa miaka minne mfurulizo na kuwapa majibu ya hatua walizochukua dhidi ya waliosababisha hali hiyo.

Wakizungumza jana kwenye mkutano wa hadhara wananchi hao wakiongozwa na Jonson Nkota mkazi wa Ichenjezya, aliosema amekuwa akifuatilia vyombo vya habari akisikia halmashauri ya Mbozi imepata hati yenye mashaka kwa miaka minne mfurulizo lakini  hajasikia hatua zikichukuliwa kwa wahusika.

Alisema halmashauri za wilaya zingine zimekuwa zikiwafukuza kazi wakurugenzi,maafisa utumishi,manunuzi pamoja na watumishi wengine kutokana na kushindwa kuwajibika na ndiyo maana zimekuwa zikipata hati safi lakini halmashauri ya Mbozi imegeuka shamba la bibi.

‘’Haiwezekani kila mwaka tupate hati chafu wakati tunavyanzo lukuki vya mapato halafu hakuna hatua zinazochukuliwa kwa wanaosababisha hali hiyo,tunakuomba mbunge ukae na wabunge wenzako mtupe majibu sababu ya kupata hati chafu na hatua walizochukua kwa waliosababisha’’alisema Nkota.

Akijibu hoja hizo,Mbunge wa jimbo la Vwawa Japhet Hasunga alisema,hoja za wananchi ni sahihi lakini halmashauri hiyo,imekuwa ikipata hati zenye mashaka miaka minne mfurulizo lakini si hati chafu,na kuwa hati za mashaka ni zenye mapungufu.

Hasunga ambaye pia ni mjumbe wa kamati ya bajeti katika bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania,alikiri kuwa katika halmashauri ya wilaya ya Mbozi,hali si shwari kitendo cha kupata hati za mashaka ni tatizo wakati Mbozi ni tajiri lakini usimamizi si mzuri.

Alisema halmashauri zingine huo zinathamanisha mali zake kila baada ya miaka mitatu lakini Mbozi haijawahi kufanya hivyo ndiyo sababu ya kupata hati za mashaka na kuwa alitamani kuhudhuria kikao kijacho lakini jumapili anakwenda Dodoma kupitia mahesabu ya taasisi zote kupitia kamati yake.

Hasunga alimaliza kwa kuwaahidi  wananchi wa Mbozi kuwa suala la upatikanaji wa hati za mashaka katika wilaya hiyo haitajitokeza tena na kuwataka wawe watulivu wazidi kuwaamini wabunge wao pamoja na madiwani kwa kushirikiana na watendaji na kwamba wamejipanga vizuri.

Aidha Edward Kalinga mkazi wa Hasanga alisema taarifa za hati za mashaka zimekuwa zikiwaletea hofu kubwa hasa ikizingatiwa kwamba kuna baadhi ya miradi ambayo fedha zilitolewa na hazikufanya kazi iliyokusudia alitoa mano zaidi ya S. milioni 135 zilizotoea ka ajili ya kujenga mabara lakini azikuanya kazi iliyokusudiwa

No comments:

Post a Comment