Na Ibrahim Yassin,Kyela
BIBI kikongwe mmoja Mkazi wa
kijiji cha kanemele kata ya lusungo wilayani Kyela mkoani
Mbeya Veronica Kanemele (75) amevamiwana watu wasio julikana
nyumbani kwake usiku wa manane na kukatwa
mkono wa kushoto na kitu chenye ncha kali kakutokana
na kile kinachodaiwa kuwa ni imani za
kishirikina.
Mashuhuda wa tukio hilo walikiambia gazeti hili kuwa tukio hilo la kushangaza lilitokea usiku wa manane wakati bibi huyo akiwa amelala fofo nyumbani kwake , ambapo bila kujua hili wala lile alijikuta akikatwa mkono wake wa kushoto uliopelekea kunyofoka na kusemawanashangaakutokana na tukio hilo kuwa la kwanza kutokea maeneo hayo.
Walisema baada ya kusikia bibi huyo akipiga mayowe ya kuomba msaada ndipo walijitokeza waliamua kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa kitongoji hicho ambae alifika mapema na kutoa taarifa kwa uongozi ngazi ya juu ambao ulifika eneo la tukio na kutoa taarifa polisi.
Akizungumzia tukio hilo kwa masikitiko makubwa mwenyekiti wa kitongoji cha Bugogo,Zakaria Ngasa alisema baada ya kuwasili eneola tukio alifanya jitihada za kumkimbiza hospital ya Matemakwa ajili ya matibabu kutokana na kwamba mkono wake ulikuwa umekatwa na kunig’inia na kupelekea madakitari kuunyofoa mkono huo baada ya kushindikana kuungwa.
Kwa upande wake Diwani wa kata hiyo,Veronika Kanyanyila alikirikutokea kwa tukio hilo na kusema kitendo hicho kimewasikitisha wananchi na ameitaka jamii kuliachia jeshi la polisi kufanya kazi yake na kuwasaka waalifu popote walipo ili wachukuliwe hatua za kisheria.
Alisema kijiji hakiwezi kuwashinda watu walio na imani potofu za kishirikina na kufanya matukio hayo , na kuwaomba wananchi kushirikiana kwa pamoja na jeshi la polisi ili kuweza kuwanasa watuhumiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria .
Alisema ifike wakati watu waweze kumwogopa mungu kwani kufanya vitendo hivyo kuna fanya watu kuwa na hofu husani wazee vikongwe kuishi bila amani kutokana na uwepo wa matukio hayo.
Mkuu wa jeshi la polisi wilayani kyela Amiri Mahamba alisema amepata taarifa ya tukio hilo na ametuma askari kwa ajili ya kuchunguza na atatoa ufafanuzi zaidi baada ya kupata taarifa za kina juu ya tukio hilo.
Mashuhuda wa tukio hilo walikiambia gazeti hili kuwa tukio hilo la kushangaza lilitokea usiku wa manane wakati bibi huyo akiwa amelala fofo nyumbani kwake , ambapo bila kujua hili wala lile alijikuta akikatwa mkono wake wa kushoto uliopelekea kunyofoka na kusemawanashangaakutokana na tukio hilo kuwa la kwanza kutokea maeneo hayo.
Walisema baada ya kusikia bibi huyo akipiga mayowe ya kuomba msaada ndipo walijitokeza waliamua kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa kitongoji hicho ambae alifika mapema na kutoa taarifa kwa uongozi ngazi ya juu ambao ulifika eneo la tukio na kutoa taarifa polisi.
Akizungumzia tukio hilo kwa masikitiko makubwa mwenyekiti wa kitongoji cha Bugogo,Zakaria Ngasa alisema baada ya kuwasili eneola tukio alifanya jitihada za kumkimbiza hospital ya Matemakwa ajili ya matibabu kutokana na kwamba mkono wake ulikuwa umekatwa na kunig’inia na kupelekea madakitari kuunyofoa mkono huo baada ya kushindikana kuungwa.
Kwa upande wake Diwani wa kata hiyo,Veronika Kanyanyila alikirikutokea kwa tukio hilo na kusema kitendo hicho kimewasikitisha wananchi na ameitaka jamii kuliachia jeshi la polisi kufanya kazi yake na kuwasaka waalifu popote walipo ili wachukuliwe hatua za kisheria.
Alisema kijiji hakiwezi kuwashinda watu walio na imani potofu za kishirikina na kufanya matukio hayo , na kuwaomba wananchi kushirikiana kwa pamoja na jeshi la polisi ili kuweza kuwanasa watuhumiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria .
Alisema ifike wakati watu waweze kumwogopa mungu kwani kufanya vitendo hivyo kuna fanya watu kuwa na hofu husani wazee vikongwe kuishi bila amani kutokana na uwepo wa matukio hayo.
Mkuu wa jeshi la polisi wilayani kyela Amiri Mahamba alisema amepata taarifa ya tukio hilo na ametuma askari kwa ajili ya kuchunguza na atatoa ufafanuzi zaidi baada ya kupata taarifa za kina juu ya tukio hilo.
Kamanda wa polis mkoani Mbeya Dhahiri Kidavashari
amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa jashi lake linaendelea na
uchunguzi wa kuwasaka wahusika wa tukio hilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment