MDHIBITI
mkuu wa hesabu za serikali (CAG) ameliambia Baraza la Madiwani wa halmashauri
ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe sababu kubwa nne zilizosababisha halmashauri
hiyo kupata hati yenye shaka katika hesabu za mwaka wa fedha wa 2014/2015 na
miaka mitatu mingine ya nyuma.
Akizungumza
jana kwenye kikao cha baraza hilo kilichokutana kupitia hoja za ukaguzi
mwakilishi wa CAG mkoani hapa Deogratus Njau alisema sababu zilizosababisha hati ya mashaka ni
pamoja na kutotenganisha mali za kudumu ardhi na majengo kama matakwa ya kanuni
za kihasibu zinavyotaka, kutoonesha thamani ya mali za kudumu katika hesabu.
Aliendelea
kueleza sababu nyingine kuwa ni kutoonesha thamani halisi ya ardhi kwenye
hesabu hizo na kushindwa kuonesha hasara ya thamani ya fedha kiasi cha Sh.
410,755,546.97 ambayo haikuoneshwa ipasavyo kwenye hesabu za mwisho kwa sababu
hesabu za mwaka 2012/2013 zilijumuisha mali za kudumu, mapato na matumizi ya
halmashauri ya mji wa Tunduma ambapo fedha hizo zilitakiwa zionekane huko kwani
walitakiwa kutengeneza hesabu zao.
Njau
alieleza mtiririko wa hati zilizotolewa kwa halmashauri ya wilaya ya Mbozi
katik kipindi cha miaka minne kuwa mwaka 2011/2012 ilipata hati ya mashaka,
2012/2013 ilipata hati yenye mashaka, 2013/2014 hati inayoridhisha na mwaka
2014/2015 hati yenye mashaka.
Aidha
ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za serikali imetoa ushauri na
mapendekezo ya jumla kwa halmashauri hiyo kuwa iongeze juhudi zaidi ya
utekelezaji wa mapendekezo ya hoja yaliyobakia, kutofanya hivyo kutasababisha
kujirudia kwa mapungufu hayo, kuimarisha utoaji huduma , matumizi mabaya ya
mali za umma na usimamizi wa fedha na udhibiti usio na ufanisi wa rasilimali .
Kwa
upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya Mbozi Edina Mwaigomole
alisema halmashauri yake inakabiliwa na upungufu mkubwa wa watumishi ambao
umesababishwa na mgawanyo wa halmashauri mbili za Momba na Tunduma ambapo
watumishi waligawanywa kutoka halmashauri mama ya Mbozi hali inayosababisha kazi nyingi
kukwama.
Alitoa
mfano kazi ya kuthaminisha ardhi haikuweza kufanyika kutokana na kukosa
wathamini ambapo pia idara ya ardhi haina mpima ambaye anatakiwa kupima ardhi,
pia aliitaja idara ya ujenzi kuwa inakabiliwa na upungufu mkubwa na wataalamu
hivyo kuiomba serikali kuwapatia wataalamu ili kuongeza ufanisi.
Akichangia
hoja katika kikao hicho Diwani wa kata ya Mpito Richard Mahaya alisema baadhi ya madeni hayajawahi kuletwa katika
vikao vya kawaida lakini wanashangaa leo kuyaona katika hesabu za ukaguzi na
kuwa yangeletwa katika vikao vya kawaida yangetafutwa ufumbuzi kuliko kuyaacha
yakasababisha hoja za ukaguzi.
Alisema
wakati wa kugawanya wilaya mbli za Momba na Mbozi waligawa mali na madeni
lakini alishangaa kuopna baadhi ya madeni ya momba kuonekana katika hesabu hizo
jambo ambalo linaongeza hoja zisizo za msingi alipendekeza ziondolewe.
Mmoja
ya wananchi waliofika kusikiliza kikao hicho
Frank Mwilenga alishangazwa na ukimywa ya viongozi kuhusu zaidiya Sh.
410milioni ambazo zimekuwa zikibishaniwa muda mrefu kutoeleza ukweli kama fedha
hizo ni mali ya halmashauri ya mji wa Tunduma mapema hli iliyosababisha kuundwa
Tume ya kuzifuatilia.
Mwisho
No comments:
Post a Comment