Stephano Simbeye,Mbozi
VWAWA: Wajumbe wa halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi
(CCM) wilaya ya Mbozi mkoani Songwe wamewavua madaraka viongozi wawili
waandamizi kwa madai ya kukigawa chama na kutozingatia maadili ya viongozi.
Uamuzi huo umetolewa jana kwenye kikao kilichofanyika katika
viwanja vya ofisi ya chama wilaya ambapo waliotimuliwa walitajwa kuwa ni Mjumbe
wa halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) George Mwenisongole na Katibu Itikadi na
uenezi wa wilaya Walen Kaminyoge.
Awali Katibu wa CCM wilayani hapa Doris Kimambo akiwasilisha
agenda ya kujadili mienendo ya viongozi wa chama hicho alisema Katibu Itikadi
na uenezi Walen Kaminyoge amekuwa anatoa
siri za chama na tabia isiyo ridhisha kwenye jamii na ambayo inakidhalilisha
chama ya ulevi huku akikopa vinywaji ambapo chama kimemlipia mara mbili ili kuondoa
fedhaha kwa kiongozi wake.
Alisema suala hilo limezungumzwa katika ngazi za awali na
kuwa bado hajabadilika na hivyo kuamua kulepeleka katika kikao hicho ambacho ni
kikubwa Zaidi ili kiweze kulijadili na kulitolea maamuzi na ambacho ndicho
chenye jukumu la kuangalia mienendo ya wanachama.
Baada ya kuanzisha hoja hiyo alisimama mjumbe mmoja Edward
Mwamundi ambaye alidai kuwa ni kweli mwenezi huyo anakiaibisha chama , lakini
alihoji kuwa kuna kiongozi mmoja ameachwa ambaye ni MNEC nayeye ajadiliwe
katika kikao hicho jambo ambalo liliungwa mkono na wajumbe wengine.
“ ndugu mwenyekiti inavyoonesha mtu mwenye fedha mnamuogopa
na hachukuliwi hatua zozote kwani tumekuwa na mgogoro na Mjumbe wa Halmashauri
Kuu ya Taifa (MNEC) muda mrefu naye huyu hatufai mbona hamjaleta hoja yake hapa
” alihoji Mwamundi.
Alisema Mjumbe wa halmashauri kuu anakigawa chama kwa
kutumia uwezo wa fedha alizo nazo , amekuwa akitumia lugha ya matusi ya nguoni kwa
viongozi wake pia wakati wa uchaguzi aliahidi anamwangusha aliyekuwa Mbunge wa
Mbozi na amefanikiwa kufanya hivyo.
Hata hivyo baada ya wajumbe kuunga mkono hoja ya mjumbe
mwenzao Mwenyekiti wa Chama wilaya ya Mbozi Aloyce Mdalavuma aliwahoji wajumbe
kuhusu hoja ya kumjadili MNEC ambapo wajumbe walikubali na kuanza kumjadili.
Katibu wa chama hicho Doric Kimambo alitowa mwongozi alisema kuhusu MNEC zipo taratibu stahiki zinazopaswa kufuatwa
kama zilivyofanyika kwa Katibu Mwenezi jambo ambalo wajumbe walimkatalia.
Akizungumza kwa njia ya simu Katibu Itikadi na uenezi Walen
Kaminyoge alisema bado hajapata taarifa ya kiofisi na kwamba mara atakapopata
ujumbe huo ndipo atakuwa na jambo la kuzungumza ingawa alisema kikao hicho
ndiyo waajili wake hivyo hawezi kurumbana nao.
Alisema pamoja na kuwa amaheshimu maamuzi ya kikao lakini
bado kanuni hazijafuatwa kwa kupewa nafasi ya kujitetea.
Naye mjumbe wa Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa
(NEC) George Mwanisongole akizungumza
kwa njia ya simu alikiri kupata taarifa isiyo rasmi kuhusu maamuzi hayo lakini
alisema kikao kilichofanya maamuzi hayo ni batili kutokana na kuwa baadhi ya
wajumbe walihongwa kushawishi wajumbe wenzao na wengine hawakuwa wajumbe halali
wa kikao.
Alisema katika kikao hicho hapakuwa na ajenda ya kumjadili
yeye bali kuna baadhi ya viongozi ambao anapingana nao kisiasa ndiyo waliotoa
fedha kuwahonga wajumbe wasiozidi saba ambao walijenga ushawishi hadi hoja ya kumjadili ikaingizwa kwenye kikao.
Kuhusu madai ya kuwa anakigawa chama alisema hajaelewa maana
yake kwa kuwa baadhi ya mambo yaliyodaiwa kwenye kikao hicho ni ya muda mrefu
na yalikwishapatiwa ufumbuzi na kuwa hakuna wanachama ambao yeye amewagawa.
Mwisho
No comments:
Post a Comment