Social Icons

Friday, 14 October 2016

Galawa Awataka Wanasoingwe Kuimarisha Umoja Kumuenzi Mwalimu Nyerere


Stephano Simbeye




MBOZI:Wananchi mkoani Songwe wameaswa kuepuka migogoro isiyo kuwa na tija badala yake waimalishe umoja na mshikamano na kufanya kazi kwa bidii na maarifa kila mmoja kwa nafasi yake katika kuenzi yale aliyo yapigania Mwl.Nyerere.

Wito huo umetolewa na leo na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Luteni Mstaafu Chiku Galawa katika maadhimisho ya miaka 17 tangu kufariki Mwassisi wa Taifa hili na Rais wa kwanza wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Julius Kambarage Nyerere iliyo fanyika mjini Vwawa wilayani Mbozi Mkoa hapa kuwa wasipoteze muda kushughulikia mambo yasiyo ya msingi

 Alisema kuendekeza migongano kutachelewesha maendeleo,kwani badala ya kufanya kazi muda mwingi utapotea kushughulikia migogoro jambo ambalo halitakuwa na tija yoyote bali kwa pamoja wajipange kufanya kazi na wasikubali maneno ya kuwagawa.

 Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ameongeza kwa kulaan watu wanao haribu mazingira kuwa hao hawalitakii mema Taifa hili kwani uhalibifu wao utaleta jangwa ambalo litasababisha mvua ikakosekana.

 Awali Mzee maarufu na ambaye Pia alikuwa mwenyekiti wa kwanza wa Halmashauri ya wilaya ya Mbozi Mzee Nelsen Mwampashe amesema mfumo wa vyama vingi vya siasa ulianzishwa na Nyerere ili viweze kuikosoa serikali iliyopo madalakani ili ijisahishe.

 Naye Mwenyekiti wa mamwene wilayani hapa Chifu Mleshelwa Nzuda alisema anamkumbuka Nyerere kwa kuondoa ukabila ambapo alisema kabla ya hapo ilikuwa vigumu kabila lingine kuja kulima katika ardhi yao jambo ambalo kwa sasa halipo tena, na kwamba yeye kama chifu ana mke wa kabila lingine na wanaishi vizuri.

No comments:

Post a Comment