Stephano Simbeye,
MBOZI:
Mkazi
wa kijiji cha Utambalila wilayani Mbozi mkoani Songwe Daimon Simchimba (68)amekufa
baada ya kupigwa na kitu kizito kichwani na Huruma Mwashiuya (38) mkazi wa
kijiji hicho, anayedaiwa kuwa mtumiaji wa dawa za kulevya aina ya Bangi.
Ofisa
mtendaji kijiji cha Utambalila Felix Mwampashe alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana saa
3.00 asubuhi wakati marehemu huyo akielekea kwenye shughuli zake za shamba
ndipo aliviziwa na muuaji ambaye alimpiga na kitu kizito kichwani na
kusababisha kifo hicho.
Alisema
taarifa za mauaji hayo zilitolewa na mtoto wa muuaji ambaye alipiga yowe kuomba
msaada ndipo wanakijiji walipojitokeza na kumzingira na kumweka chini ya ulinzi
na kisha kumfikisha katika ofisi ya kijiji ambapo walipomhoji alikataa kusema
chochote akidai atakwenda kueleza mbele ya safari sababu za mauaji hayo.
Kamanda wa
Polisi mkoani hapa Mathias Nyange amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwa
mtuhumiwa wa mauaji hayo anashikiriwa na jeshi hilo na kuwa bado chanzo cha
mauaji hayo hakijafahamika na kwamba uchunguzi wa awali unaonesha kuwa
mtuhumiwa ni mvutaji wa bangi iliyomfanya kuchanganyikiwa na kufanya kitendo
hicho cha kikatili.
Wakati huo
huo Kamanda Nyange amesema mtu mmoja mkazi wa mtaa wa Ipito katika Halmashauri
ya mji wa Tunduma Musa Sanga (54) amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kamba
ya manila baada ya kukelwa na kuugua
ugonjwa wa kisukari muda mrefu.
Tukio hilo
limetokea jana saa 11:40 jioni ambapo mwili wa marehemu ulikutwa unaning’inia
ndani ya nyumba yake huko katika kitongji cha Ipito katika kata ya Mpande,
Tunduma mkoani Songwe.
Aidha hivi
karibuni Kamnda Nyange alikaririwa akisema kila baada ya saa sita linaripotiwa
tukio moja la mauaji katika mkoa wa Songwe kutokana na imani za kishirikina,
wivu wa mapenzi na migogoro ya ardhi.
Mwisho
No comments:
Post a Comment