Social Icons

Monday, 3 October 2016

Timu ya Kimondo Yalazimishwa Sale ya bila kufungana




Stephano Simbeye, 

Timu ya Soka ya Kimondo SSC ya mkoa wa Songwe jana ilitoka sale  ya bila kufungana katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Coastal Union ya Tanga, katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa CCM Vwawa wilayani Mbozi.

Katika mchezo huo ambao ulianza kwa kila timu kujihami kwa kucheza kwa tahadhari kubwa  huku timu ya Kimondo ikishuhudia kosakosa nyingi langoni mwa lango la wapinzani wao kutokana na washambuliaji wake kutokuwa makini.

Kipindi cha Kwanza dakika 45 timu ya Kimondo ililisakama mara kadhaa lango la mpinzani wake lakini ilionekana washambuliaji wake kuwa butu baada ya kushindwa kuliona lango licha ya kuwa walitawala kila idara wakiichezesha mchakamchaka timu hiyo ya wagosi wa kaya.

Baada ya timu ya kimondo kutakata wakicheza soka safi licha ya kushindwa kuliona lango,timu ya wagosi wa kaya walianza kujihami wakichelewesha mipira na kujiangusha mara kadhaa wakitaka wapate sare, hivyo hadi mwamuzi wa mchezo huo Misheki Suda kutoka  Singida anapuliza kipenga cha  dakika 90 kumalizika timu hizo zilikuwa hazijafungana.

Akizungumza na waandishi wa habari,kapteni wa timu ya Costal Union,Mbwana Hamis alisema wamejitahidi kutoka sare maana mpira ulikuwa mgumu hasa uwanja ulivyo kuwa mbovu ulichangia wao kupwaya na kuwa mechi ijayo watajipanga ili washinde.

Kocha wa timu ya Kimondo,Fulgence Novatus alisema vijana wake walicheza vizuri ila walikosa umakini,tatizo ni umaliziaji,huku kocha wa Costal Mohammed Kampira alikiri kuwa walitingwa na kusema wanajipanga mechi ijayo watahakikisha wanashinda.

Mkurugenzi wa timu ya Kimondo SSC, Elick Ambakisye,alisema wameliona tatizo la timu yake ni umaliziaji kwa kuwa kocha ameliona atalifanyia kazi na kuwa wachezaji wengi muhimu walikuwa majeruhi walipocheza na timu za Malawi na Zambia katika michezo ya majaribio hivyo mechi zijazo anaamini watafanya vizuri.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment