Stephano
Simbeye,
VWAWA:Wazo
la kutaka kuipandisha hadhi hospitali ya wilaya ya Mbozi (Vwawa) kuwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Songwe
limekataliwa na Baraza la Madiwani wa Halmashauri wilayani hapa na kutaka wazo hilo lielekezwe
katika hospitali ya Misheni Mbozi.
Uamuzi huo ulitolewa
mwishoni mwa wiki wakati wa kikao cha dharura cha madiwani hao ambao walidai
kuwa wazo hilo ni zuri Lakini lielekezwe kwenye hospitali ya Misheni ya Mbozi
inayomilikiwa na Kanisa la Moravian jimbo la Kusini Magharibi kutokana na kuwa
katika hospitali ya wilaya kuna majengo machache pia hakuna eneo litakaloruhusu
upanuzi.
Diwani wa
kata ya Mpito Richard Mahawa (CCM) alisema katika hospitali ya wilaya
palipofikiriwa kuwa hospitali ya mkoa hapafai kwa vile eneo lake ni dogo ambalo
haliwezi kukidhi mahitaji yanayotakiwa kuwa hospitali ya mkoa.
Diwani wa
kata ya Igamba Exaud Kibona alisema kutokana na mazingira yalivyo katika
hospitali ya Misheni Mbozi yanakidhi kutumika kuwa hospitali ya rufaa ya mkoa
ukianzia katika miundombinu ya barabara, majengo na pia kuna nafasi ya kutosha
kwa ajili ya upanuzi.
Awali Kaimu
Katibu Tawala mkoani hapa Erick Mapunda aliwartaka madiwani hao kuridhia
mapendekezo ya mkoa ya kutaka kuipandisha hospitali hiyo kuwa ya mkoa ili
Serikali iweze kuongezea bajeti ya kuihudumia, pia italeta madaktari bingwa na
vifaa tiba kuliko ilivyo hivi sasa.
“ hii ni
fursa nawaomba waheshimiwa madiwani ipokeeni ili Serikali iweze kutia mkono
wake kwani itaongeza bajeti yake na kuboresha miundo mbinu ili iweze kuendana
na mahitaji halisi ya hospitali ya mkoa, na kwamba mawazo waliyo nayo
wayatafakari kwa kina kwani ni vigumu kuboresha kwenye nyumba ya mwingine
badala ya nyumbani”alisema Mapunda.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbozi Elick Ambakisye alisema wazo
ni jema Lakini halikufuata utaratibu kwa wazo kuanzia juu badala ya kuanzia
ngazi ya chini badala ya hatua zilizochukuliwa hivi sasa za kuanza mchakato
pasipo kuihusisha Halmashauri yake.
“ hapa
tunaona kama wazo hili lisingerudishwa kwetu na wizara lingekuwa limefika mbali
jambo ambalo linaleta msigano usiokuwa wa lazima, tunakuomba mwakilishi wa RAS
fikisha salaam, tunahitaji kushirikiana sote tuujenge mkoa Lakini si hivi
mnavyotaka kufanya”Alisema Ambakisye
Msemaji wa
Kanisa la Moravian Jimbo la Kusini Magharibi Mchungaji Zakaria Sichone
akizungumza kwa njia ya simu amesema bado hawajapokea ombi la kutaka
kuipandisha hadhi hospitali yao kuwa ya rufaa ya mkoa, Lakini alisema iwapo
ombi hilo litawasilishwa litafanyiwa kazi kwa kupelekwa katika vikao husika.
Alisema hospitali
ni huduma ya wananchi ambapo wazo la kuipoandisha hadhi si tofauti na lengo
lililokusudiwa tan gu awali hivyo Kanisa halitakuwa na kipingamizi chochote
iwapo Serikali imeamua kuitumia hospitali hiyo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment