Na
Ibrahim Yassin,Kyela
KATIKA
hali isiyokuwa ya kawaida mkazi wa kijiji cha Kafundo kata ya Ipinda tarafa ya
Ntebela wilayani Kyela Mbeya,Stephen Emmanuel amefariki dunia kwa kuchomwa na kisu maeneo kadhaa katika mwili wake na kijana ambaye ni mkazi wa Iringa ambaye
jina lake halikufahamika.
Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni rafiki wa marehemu,Alimoni
Mwanjasi mkazi wa Lufilyo halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe,alisema wakati wa tukio
marehemu Emmanuel alikuwa na mdogo wake,Samwel Emmanuel wakinywa pombe
kilabuni.
Alisema
wakati wanakunywa pombe katika virabu vya Ipinda mjini,kaka wa marehemu alikuwa
amevaa skafu ya chadema ndipo alipotokea kijana huyo mkazi wa Iringa aliyefika
kijijini humo kwa kazi za ujenzi wa nyumba aliomba apewe skafu kwa kuwa
aliipenda.
Alisema
baada ya kutopewa Samwel aliinuka kwenda kujisaidia haja ndogo,wakati anatoka
kijana huyo alimfuata na kumpiga visu vya shingoni,mkononi na kichwani ambapo
mdogo mtu aitwaye Stephen alifika kumsaidia kaka yake ndipo alipopigwa visu
maeneo kadhaa na kupoteza fahamu.
Aliongeza
kuwa baada ya hapo watu walijaa maeneo hayo wakitaka kuchukua sheria mkononi
kwa kutaka kumuua ambapo jeshi la polisi lilifika eneo hilo na kutuliza ghasia
na kumchukua mtuhumiwa kumpeleka polisi na majeruhi kupelekwa kituo cha afya
Ipinda.
Mwanjasi
alisema majeruhi akiwa kituo cha afya alifanyiwa huduma za matibabu na kushonwa
sehemu alizochomwa visu lakini baada ya dakika kumi alifariki dunia na kumbeba
hadi kijijini kwao Kafundo kwa taratibu za maziko.
Aliongeza
kuwa yeye ni mkazi wa kijiji cha Lufilyo Busokelo anafanya kazi ya umachinga
huku kijana aliyefariki alikuwa akimsaidia kazi za kuuza na kuzungusha bidhaa
zake kabla ya kukutwa na umauti akiwa kirabuni na kaka yake akinywa pombe.
John
Ambike Mwenyekiti wa kitongoji cha Kafundo,katika maziko ya kijana huyo
yaliyofanyika leo,alisema wao kama wananchi wapo sambamba na familia ya
marehemu kuhakikisha sheria inafuatwa kwa kuwa kitendo kilichofanyika ni kosa
la jinai.
Alisema
kaka wa marehemu ambaye naye alijeruhiwa kwa kuchomwa vifu alitibiwa na
kuruhusiwa kurudi nyumbani huku hali yake ikiendelea vizuri.
Hata
hivyo jina la mtuhumiwa wa mauaji hayo halikuweza kufahamika ambapo
juhudi za kulipata jina hilo zitakamilika pindi atakapo pandishwa
kizimbani.
Kamanda
wa polisi mkoani Mbeya Dhahiri Kidavashari,alithibitisha kutokea tukio hilo na kuwa jeshi la polisi limemkamata
mtuhumiwa huyo ambaye bado hajapewa jina lake kutokana na kuwa ni mgeni
katika kijiji hicho na kuwa uchunguzi unaendelea kabla ya mtuhumiwa kupelekwa
mahakani.
No comments:
Post a Comment