Social Icons

Tuesday, 25 October 2016

Wajumbe wa Baraza la Mji wagoma kuendelea na kikao

Stephano Simbeye, Mbozi

Wajumbe wa Baraza la Mamlaka ya mji mdogo wa Vwawa jana  waligoma kuendelea na kikao cha baraza hilo ikiwa ni njia ya kushinikiza halmashauri ya wilaya Mbozi mkoani Songwe kurejesha zaidi ya Sh. 126milioni ambazo zingejenga matundu 32 ya vyoo, vyumba sita vya madarasa , ilizotumia bila ridhaa yake hivyo kufanya miradi hiyo kukwama .
 
Akizungumza mapema wakati wa kuridhia ajenda za kikao hicho ambacho kilikua cha kawaida mmoja ya wajumbe hao  Yaled Mtafya aliomba mwongozo kuhusu utekelezaji wa  maazimio ya baraza la dharura lililokaa Septemba 27 mwaka huu na kutoa maazimio ya kutaka hamashauri ya wilaya iwapatie kiasi hicho cha fedha na kwamba isipofanya hivyo wajachukua hatuwa ya kurudi kwa wananchi na kuwataka wasilipe tozo zozote za mamlaka hiyo hadi hapo fedha hizo zitakapopatiana   
 
Alisema kwa muda mrefu sasa mamlaka ya mji haijafanya sughuli yoyote ya maendeleo kutokana na fedha za makusanyo yake zimehodhiwa na halmashauri na jitihada za kufuatilia  hazijazaa matunda hali iliyofanya kamati ya fedha kwenda kwa mkuu wa wilaya ambaye naye  amedhalauliwa kutokana na kutotekeleza maagizo yake.
 
Mwenyekiti wa mamlaka ya mji wa Vwawa  Ephraim Mwakateba aliitaja baadhi ya miradi iliyokwama kutokana na kukosekana kwa fedha hizo kuwa ni pamoja na ujenzi wa matundu 32 ya vyoo katika shule za msingi za Ilolo na seondari Vwawa, vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Mtumbo, vyumba vya madarasa 8 na ujenzi wa shule mpya ya kidato cha tano katika kata ya hasanga na kazi ya uzoaji taka katika maeneo mbalimbali ya mji.
 
Alisema chanzo cha mgogoro huo ni agizo la serikali kutaka akaunti za mamlaka zifungwe na kuanza kuingiza makusanyo yatokanayo na vyanzo vya mapato yake katika akaunti za halmasauri ya wilaya jambo ambalo linaonesha halmashauri  imezitumia fedha hizo kwa matumizi mengine bila ridhaa ya wenye fedha hivyo kusababisha usumbufu zinapohitajika
 
Mwakateba Alisema azimio la kugoma kuendelea na kikao hicho linatokana na kucheleweshwa kwa fedha za Mamlaka ambazo zilikuwa zikiingizwa kwenye akaunti ya halmashauri kwa agizo la serikali na kwamba iwapo fedha hizo hazitarejeshwa wanatoa siku saba kwa halmashauri iwe imelipa fedha hizo vinginevyo watafanya mikutano ya hadhara kuwakataza wananchi wasitoe malipo yoyote hadi hapo suala hili litakapoisha na ikibidi watakwenda kumuona Waziri wa Tamisemi George Simbachawene
 
Akizungumza kwenye kikao hicho kabla ya kuvunjika Afisa Mtendaji Mkuu wa mamlaka hiyo Joel Kaminyoge aliwataka wajumbe hao kubadili msimamo wao kwani utekelezaji wa maazimio ya kikao chao cha dharura cha Septemba 27 mwaka huu, umeanza baada ya halmashauri kuanza kulipa fedha zao ikiwa ni pamoja na Sh. 26 milioni, malipo ya Sh. 18 milioni yamekamilika na malipo mengine ya Sh. 8.8 yanakaribia kukamilika.
 
Kaminyoge alisema tofauti na huko nyuma ambapo kwa mwezi zilikuwa zinalipwa Sh. 1 milioni kwa mwezi lakini sasa kazi imeongezeka hivyo kuwaomba madiwani kusubiri hatua alizoanza kuzichukua.
 
“ waheshimiwa wajumbe tusubiri kiongozi wetu akamilishe jitihada zake za kutusaidia kupata fedha zetu na hapa mmesikia kuwa ameagiza kwamba kabla ya Novemba 4 mwaka huu awe amepelekewa mchanganuo wa namna ya kulipa kwa maandishi” alisema Kaminyoge
 
Awali akitoa salamu za serikali Mkuu wa wilaya ya Mbozi John Palingo aliwataka wajumbe wa Mamlaka ya mji kuzitumia fedha hizo kwenye miradi ya maendeleo ambayo hawajaitekeleza kwa muda wa mwaka mzima.
Mwisho.
 

No comments:

Post a Comment