Stephano Simbeye,
Tunduma: Madereva wa mabasi madogo yanayofanya safari kati
ya Tunduma, na Mpemba wilaya ya Momba mkoani Songwe, wametishia kusitisha
huduma hiyo kufuatia madai ya kunyanyaswa na askari wa usalama barabarani kwa
kuwatoza faini nyingi zisizokuwa na msingi na kuwataka kulipia faini hizo kwa
njia ya M pesa.
Wakizungumza jana
katika mahojiano na waandishi wa habari baadhi ya madereva hao waliokutwa
katika kituo kikuu cha mabasi mjini Tunduma walidai kuwa askari hao wa usalama barabarani
wamekuwa wakiwakamata kila wanapowaona na kuwaandikia karatasi za kulipa fain (notification)
na iwapo wakiwadai stakabadhi wanawabambikizia makosa mengine.
Mmoja wa madereva hao Ayub John aliyataja makosa ambayo
wanakamatwa nayo kuwa ni pamoja na kuzidisha abiria (Level seat) jambo ambalo
kwa biashara ya safari fupi ni hasara kutokana na kuwa mabasi hayo madogo
yanabeba abiria wachache na nauli yake ni ndogo ya Sh. 500 hivyo iwapo
wakipakia abiria 11 hadi 17 kipato
wanachopata ni kidogo ukilinganisha na gharama za mafuta kiasi ambacho ni
hasara.
Dereva Baton Tumbope alisema iwapo hali hii itaendelea
watalazimika kusitisha huduma hiyo kwa kuwa wanaona kazi haiwapatii faida
tokana na kero hiyo na kuliomba jeshi la polisi kukaa nao ili kuweka sawa mambo.
“Sisi madereva wa daradara tunanyanyasika na askari wa usalama
barbarani wametufanya chanzo cha mapato yao wakati Fulani wanataka tuwaingizie
fedha za faini kupitia simu kwa njia ya M pesa na ukihoji kwanini imekuwa hivyo
unawekwa mahabusu” alisema Baton Tumbopee
Kiongozi wa madereva hao Patson Simbeye alisema amekuwa
akipokea malalamiko ya madereva kila wanapotoka na kurudi kwenye safari zao ya
kukamatwa hovyo na kutozwa faini jambo ambalo linawafanya washindwe kutimiza
malengo ya biashara na kufanya kazi hiyo kuwa ngumu.
Alisema kufuatia kero hiyo walikwisha peleka malalamiko yao
kwa Mkuu wa mkoa wa Songwe na Kamanda wa polisi mkoani hapa lakini bado
hayajafanyiwa kazi bado kero hiyo inaendelea.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoani hapa Mathias Nyange
alisema polisi wanafanya kazi zao vizuri kwa kusimamia sheria zilizopo vizuri
hata hivyo aliwasihi madereva hao kwa mwenye ushahidi wa kutakiwa kutuma fedha
za faini kwa njia ya mpesa waupeleke ili hatua zichukuliwe dhidi ya askari huyo
kwani huo sio utaratibu wa malipo ya fedha za serikali.
“ ukiona askari wanalalamikiwa ujue wanafanya kazi zao
vizuri katika utendaji huwezi kupendwa, isipokuwa kama kuna suala la kuomba
rushwa tunaomba tupatiwe ushahidi ili askari husika achukuliwe hatua za
kinidhamu kwa mujibu wa sheria” alisema Kamanda Nyange
Mwisho.
Stephano Simbeye
Tunduma: Jeshi la polisi mkoani Songwe limekamata kete 200
za madawa ya kulevya aina ya heroin ambayo thamani yake bado haijajulikana katika
msako uliofanywa katika halmashauri ya mji wa Tunduma wilayani Momba.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa Mathias Nyange aliwambia jana
waandishi wa habari kuwa tukio hilo lilitokea Novemba 3 mwaka huu wakati polisi
wakifanya msako wa kubaini watumiaji na wauuzaji wa madawa hayo na kufanikiwa
kuwakamata Watoto wawili wenye umri wa
miaka 15 na 17 (majina tunayo) baada ya kukutwa na kete 20 za madawa ya kulevya
aina ya heroin
Alisema katika msako huo pia polisi walipata kete 180 za
madawa hayo yaliyokutwa katika nyumba moja ambayo mwenye madawa hayo alikimbia
kusikojulikana, thamani ya madawa hayo bado haijajulikana na kuwa jeshi hilo
linaendelea na msako kuwabaini wote wanaojihusisha na biashara hiyo haramu.
Kamanda Nyange aliongeza kuwa watu hao watafikishwa
mahakamani mara tu upelelezi utakapokamilika pia aliitaka jamii kuacha
kujihusisha na madawa ya kulevya kwani mkono wa sheria ni mrefu ambao
utawashughulikia kila kona watakayojificha.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment