Social Icons

Wednesday, 7 December 2016

TAKUKURU MKOA WA SONGWE KUENDESHA MIDAHARO

Na: Stephano Simbeye - Songwe

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Songwe inatarajia kuendesha midahalo katika wilaya zote, itakayowahusisha wananchi na wadau mbalimbali kuzungumzia kero za wananchi kuhusu rushwa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu itakayofikia kilele Desemba 10 mwaka huu.

Mkuu wa Takukuru mkoani hapa Emmanuel Kiyabo aliwaambia waandishi wa habari jana katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa mjini Vwawa kuwa, maadhimisho ya mwaka huu yatafanyika katika awamu mbili, ambapo Desemba 5 hadi desemba 8 mwaka huu katika ofisi za TAKUKURU wilaya za Ileje, Mji wa Tunduma na katika ofisi ya mkoa iliyopo Vwawa wilayani Mbozi zitasikiliza kero za wananchi dhidi ya rushwa.

Alisema awamu ya pili itahusisha midahalo itakayofanyika siku ya kilele Desemba 10 mwaka huu ambayo pia imeandaliwa na ofisi za Takukuru wilaya zote, ambapo katika ofisi ya mkoa mjini Vwawa kutakuwa na mdahalo wa vijana wa Scouts ambapo patafanyika mjadala utakaongozwa na mada isemayo “ maadili na ruswa” pia mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa mkoa wa Songwe Luteni Mtsafu Chiku Galawa.

Kiyabo aliongeza kuwa huko katika wilaya ya Ileje kutafanyika mdahalo ambapo mjadala utahusu mada isemypo“kero za usambazaji wa pembeeo za ruzku” ambapo ofisa kilimo wilyani humo atakuwepo kujibu hoja zinazohusu ugawaji wa pembejeo za ruzuku, na katika mji wa Tunduma mdahalo utauwa na mjadala usemao “ je rushwa na ukosefu wa maadili vinachangia uwepo wa migogoro ya ardhi?|”

Mkazi wa Hanseketwa wilayani Mbozi Israel Swila alisema kutoa elimu kwa wananchi juu ya namna ya kuripoti masuala ya rushwa litakuwa jambo muhimu kwani watu wengi hawajui namna na wapi mahali pa kuwasilisha kero zao has wanapoombwa rushwa ndogongogo huko vijijini waliko.

Alisema katika maeneo ya utoaji huduma kama vile ofisi za watendaji wa vijiji na kata, na mabaraza ya kata kuna ukandamizaji mwingi ambao unasababishwa na wananchi wengi utoelewa sheria mao9fisa wa maeneo husika wanatumia mwanya huo kuwanyanyasa wananchhi kwa kuwatoza rushwa.

Fatuma Mwanyula mkazi wa Nambala alisema makongamano hayo yasingoje kipindi cha maadhimisho ndipo yafanyike bali uwe utaratibu wa kila wakati ili kuwaelimisha wananchi juu ya hai zao na wajibu wao kwa ujumla ili wafahamu namna ya kuepuka kutoa rushwa na kutoa ushirikiano kwa mamlaka husika pale wanapoombwa au kuona viashiria vya rushwa.

“wakati mwingine tunafanyiwa urasimu katika huduma pasipokuombwa kitu lakini ukilitizama suala lenyewe utagundua kuwa kinachotafutwa ni kitu kidogo ili upate huduma, kwa mfano suala la ugawaqji wa mbolea za ruzuku baadhi ya watendaji huandika majina bandia ili kunufaika na baadaye kuchukua pembejeo hizo kwa manufaa yao wenyewe.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment