Social Icons

Thursday, 3 November 2016

MNEC Agoma kung'olewa

Na: Stephano Simbeye, Mbozi

Vwawa: Mjumbe wa halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC) Taifa kutoka wilaya ya Mbozi mkoani Songwe George Mwanisongole aliyeazimiwa kuvuliwa wadhifa wake huo hivi karibuni amejitokeza hadharani na kudai kuwa sababu zilizodaiwa si za kweli na kwamba yaliyojitokeza yana lengo la kumdhoofisha kisiasa. 
 
Hayo yamejitokeza siku chache baada ya wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Mbozi kumtuhumu mjumbe huyo wa NEC pamoja na katibu wa Itikadi na Uenezi (CCM) wilaya Yueni Kaminyoge waliokuwa wakituhumiwa kwa kukigawa chama, kutoa siri za chama, na kusababisha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbozi Godfrey Zambi kuanguka katika uchaguzi mkuu uliopita, huku mwenezi akituhumiwa kwa kukiuka maadili ya uongozi kwa kulewa hovyo. 
 
Baada ya kutumbuliwa Mjumbe huyo wa NEC amejitokeza hadharani na kudai kwamba sababu zilizotolewa hazina ukweli wowote bali kushindwa kwa Mbunge Zambi kulitokana na upepo wa mgombea Urais kupitia Ukawa Edward Lowasa na yeye kutokubalika kwa wananchi, pia wakati huo wanaCCM. 
 
“ mimi nilikuwa mgombea Ubunge katika kura za maoni na nilishika nafasi ya pili, ningewezaje kuwashawishi wapiga kura na kwanini nguvu hiyo nisingeepeleka kwenye kura za maoni ili kushawishi wajumbe wanichangue” alihoji Mwenisongole. 
 
Alisema tangu uchaguzi kwisha amekuwa akifanya shughuli zake za kiuchumi na kuishi Jijini Dar es salaam hivyo kuwa vigumu kuja wilayani kugawa chama, Hata hivyo Mwenisongole alisema tangu 
 
Januari mwaka huu amekuwa akigawa vifaa vya umeme jua 5000 kwa wakazi wa wilaya ya Mbozi karibu katika vijiji vyote jambo ambalo pia limemfanya ajengewe uadui na wanasiasa wenzake ambao wamekuwa wakiona kama anafanya kampeni za uchaguzi ujao. 
 
Oktoba 19 mwaka huu wajumbe wa halmashauri Kuu ya CCM wilaya waliazimia kuwa mjumbe wa NEEC taifa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wilaya waondolewe kwenye nyadhifa zao kwa madai ya kukigawa chama na ulevi wa kupindukia.
 
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Mbozi Aloyce Mdalavuma alisema jambo hilo lilijitokeza katika kikao cha halmashauri kuu ya CCM wilaya ambao walitoa uamuzi ambao ulitolewa na wajumbe wenyewe na si uamuzi wa mtu mmoja na kwamba kufuatia uamuzi huo hatua za kushughulikia jambo hilo kwa kufuata taratibu zitafuata.
 
Alisema kwa mujibu wa taratibu suala hili litapelekwe kwenye vikao vya kamati ya Siasa na hatimaye kurejeshwa tena kwenye kikao cha halmashauri  kuu wilaya kwa maamuzi na kasha suala hilo kupelekwa katika ngazi ya mkoa na hatimaye taifa kwa maamuzi ya mwisho.
Mwisho
 
Stephano Simbeye, Mbozi

Timu ya Kimondo SC ya Mbozi mkoani Songwe inayoshiriki ligi daraja la kwanza Tanzania Bara, inakabiliwa na ukata wa fedha ambao unafanya hali ya kambi ya wachezaji na viongozi wake kuwa ngumu huku mashambiki wa mchezo huo wakinyoshewa kidole kwa kutoiunga mkono timu.
 
Wakizungumza jana katika hafla fupi ya kukabidhiwa jezi zilizotolewa na Kampuni ya madini Shanta Gold Mine iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya mkuu wa mkoa wa Songwe mjini Vwawa baadhi ya wachezaji walidai kwamba wanakabiliwa na uhaba wa mahitaji muhimu ikiwemo chakula na fedha hali inayowafanya wachezaji kukosa ari.
 
Bruno Shayo ni mmoja wa wachezaji wa timu ya Kimondo alisema timu ilijiandaa vizuri lakini changamoto iliyopo ni kuwa mkoa haujaamka kimichezo ambapo wanashindwa kuiunga mkono timu hali inayosababisha wajione wakiwa.
 
“ ligi ni ya kawaida haina ushindani mkubwa  lakini kikwazo ni pesa ambapo wachezaji wanakabiliwa na uhaba wa posho za kujikimu jambo ambalo linatufanya tuwe na mawazo mengi na kukosa molari ya kucheza mpira” alisema Shayo.
 
Golikipa wa Timu ya Kimondo Joseph Mwansile aliwatupia lawama mashabiki wa mpira wilayani Mbozi kwa kushindwa kuiunga mkono timu yao, hivyo hali kutokuwa tofauti wanapocheza nyumbani na ugenini.
Kapteni wa timu hiyo Abbas Athuman alisema lengo la timu yao ni kupanda daraja ili icheze ligi Kuu msimu ujao lakini wanakabiliwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa fedha na chakula.
 
Naye mkurugenzi wa timu ya Kimondo Elick Ambakisye pamoja na kumshukuru Mkuu wa mkoa kwa Baraka zake kwa wafadhili waliotoa vifaa hivyo lakini pia alisema timu inakabiliwa na uhaba wa rasilimali fedha ambazo zinachangia kuharibu michezo.
 
“ mpera lazima unahitaji rasilimali fedha ambayo ni changamoto kubwa katika timu yake na ambayo pia imekuwa ikivuruga michezo kadhaa waliyocheza kutokana na timu washindani kuwavuruga waamuzi kwa fedha na hivyo kutokuwa na maamuzi ya haki” alisema Ambakisye.
 
Kwa upande wake kocha mkuu wa timu ya Kimondo SC Novatus Fulgence alisema wanaimarisha bechi la ufundi ili kuhakikisha timu inafanya vizuri katika michezo iliyobakia ili kufikia mkakati wao wa kupanda daraja na kucheza ligi kuu msimu ujao, licha ya kuwa timu haijaanza vizuri katika michezo ya mwanzo.
 
Msaada wa vifaa vya michezo vilivyotolewa na Kampuni ya madini ya Shanta Gold Mine ni pamoja na  Jezi jozi nne, mipira 4 na jezi za walinda mlango jozi nane vyote vikiwa na thamani ya Sh.   900000
Akizungumza katika hafla hiyo mkuu wa mkoa wa Songwe Luteni Mstaafu Chiku Galawa aliwasihi wachezaji wa timu hiyo kujituma katika mazoezi ili kufikia ndoto yao ya kushindana na wengine ili kupata mafanikio.
 Mwisho.

No comments:

Post a Comment