Social Icons

Thursday, 3 November 2016

DC. Momba Awataka Viongozi wa vijiji Kumaliza migogoro ya Wafugajio na Wakulima mapema




Na: Stephano Simbeye, Chitete

MKUU wa wilaya Momba mkoani Songwe Bw. Juma Irando amewata viongozi wa vijiji wilayani humo kutatua mapema migogoro ya wakulima na wafugaji na kujiepusha kuwa sehemu ya tatizo kwa kushawishika na tamaa ya fedha,kabla haijaleta madhala ya uvunjifu wa amani.

Alisema hayo jana wakati alipokuwa akitowa salamu za serikali katika kikao cha baraza la madiwani katika mji wa Chitete kuwa migogoro mingi ya wakulima na wafugaji husababishwa na viongozi wa vijiji na kata baadae inakuwa shida hadi kwenye ngazi ya wilaya.

“ kumekuwa na migogoro ya hapa na pale hasa ya wakulima na wafugaji tusingependa kuona migogoro hii ikiendelea na kukua bali ishughulikiwe na kumalizwa mapema pia wafugaji wasio na vibali wasiruhusiwe kwani hawa ndiyo chanzo cha migogoro” alisema mkuu huyo wa wilaya.

Bw. Irando alisema mkoa unaandaa wasifu wake ikiwemo kurasimisha ardhi yake, hivyo isingekuwa vizuri kuacha watu wengine wakiuza ardhi yao wengine wakihamahama maeneo bali jitahidini kwa nguvu zao zote kulisimamia jambo hilo.

Mmoja wa wakulima katika kijiji cha Nkara Bw. Erasmus Sinkamba alisema kumekuwa na baadhi ya viongozi wa vijiji na kata kurubuniwa na wafugaji kwa kupatiwa fedha ili kutoa ardhi kwa wafugaji ambao pia wamekuwa wakilisha mifugo yao kwenye mazao ya wakulima.

Alisema katika maneo yao tatizo hilo bado halijashamili lakini ni vizuri likachukuliwa tahadhari mapema kwani katika maeneo jirani wilayani humo tayari limekwisha anza ambapo  wafugaji wanaingia na makundi makubwa ya mifugo yao wakisaka malisho na maji.

Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo  alisema  Bw. Vedaestani  Simpassa aliwasihi madiwani na watendaji kutekeleza maagizo hayo na shughuli nyingine kwa bidii na kusahau siasa ambazo muda wake umekwisha bali wakati huu ni kutekeleza yaliyo mbele yao ili kuhakikisha wilaya yao inakuwa salama na inakwenda mbele kimaendeleo.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment