Stephano Simbeye, Mbozi
Wafanyabiashara wa mji wa
Vwawa wilayani Mbozi mkoani Songwe wametofautiana na kushindwa kuelewana na
mkuu wa mkoa huu Chiku Galawa kuhusiana na eneo la kujenga ofisi ya mkuu wa
mkoa.
Hali hiyo ilijitokeza jana katika mkutano ulioitishwa na mkuu huyo wa mkoa kwa lengo la kifahamiana ambapo mwishoni mwa mkutano huo alitowa nafasi ya kuulizwa maswali ndipo likajitokeza suala la eneo la kujenga ofisi ya mkoa ambapo baadhi ya wauliza maswali walitaka kufahamu kilichosababisha kuwepo mabadiliko tofauti na walivyotarajia.
Raphael Kibona alianza kwa kueleza
kuwa awali makao makuu ya mkoa wa Songwe yalipangwa kuwa katika kata ya Vwawa
lakini kuna mabadiliko ya eneo hilo, je ninani aliyegushi na kuyapeleka Nselewa
katika kata ya Mlowo na aliyefanye hivyo Takukuru wanamchukulia hatua zipi.
Kwa upande wake Joel Kasebele aliomba
ufafanuzi toka kwa mkuu wa mkoa kuhusu eneo la kujenga ofisi za mkoa na ni
vikao vipi vimebatilisha uamuzi wa vikao vya ngazi ya chini ambavyo viliazimia
ofisi hizo kuwa eneo la Hasamba badala yake uamuzi huo umetenguliwa.
“ kitedo cha kubadili maamuzi ya
awali kimekiuka hata taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi iliyotolewa na
Mbunge aliyepita na hapa naomba nitoe kielelezo cha taarifa hiyo”alisema
Kasebele
Naye Mwenyekiti wa wafanyabiashara
wilayani Mbozi Yohana Mwajeka alisema kuwa kwa upande wao wafanyabiashara hali
si shwali kwani walitarajia kuwa iwapo ofisi za makao makuu ya mkoa zikijengwa
katika mji huu zitasaidia kuchangamsha mji ambao umezorota kibiashara
ukilinganisha na miji mingine ya Mlowo na Tunduma.
Alisema walitarajia kuwa ofisi hizo
pamoja na nyingine za taasisi na serikali zingeweza kuongeza idadi ya watu
wanaokuja kufuata huduma ikiwa ni pamoja na watumishi wataongeza mzunguko wa
fedha ili nao waweze kupata maendeleo na kuinua uchumi wa n chi kwa ujumla.
Akijibu maswali hayo mkuu wa mkoa
Luteni Mstaafu Chiku Galawa alisema serikali inafanya kazi kwa maandishi
tangazo la serikali la kuanzisha mkoa wa Songwe limeeleza kuwa makao makuu ya
mkoa yatakuwa wilaya ya Mbozi na hapo hakuna aliyebadilisha na ndiyo maana
tumekuja Mbozi na kuwa tangazo hilo halikueleza kwa maandishi katika maeneo
hayo yanayotajwa.
Alisema tumejipanga kufanya kazi kuleta
maendeleo ya mkoa wa Songwe wenye halmashauri tano na uwa kikao cha kamati ya ushauri ya
mkoa (RCC) imeamua kujenga ofisi ya mkuu wa mkoa na si makao makuu na
tunatarajia ofisi za idara nyingine zitatawanywa maeneo mbalimbali ili kuleta
usawa ili kila mwananchi aguswe.
Galawa aliongeza kuwa mawazo ya wafanyabiashara kuwa ofisi ya mkuu wa mkoa italeta mabadiliko ya kibiashara si sahihi kutokana na kuwa ofisi hiyo ina wafanyakazi wachache ambao hawawezi kuzidi 120, jambo la msingi kwa wakazi wa Vwawa ni kufikiria namna ya kuboresha biashara zao kwa kushirikiana kwa kuunda ya kuanzisha mabaraza ya biashara ambayo yatasaidia kuwaweka pamoja.
Aidha alisema kazi ya ofisi ya mkuu wa mkoa haifanyi kazi za kila siku za kuonana na wananchi bali kazi hiyo hufanywa na halmashauri za wilaya, na kazi ya mkoa ni kusimamia wilaya na kuinua kipato cha wananchi kutoka hapo walipo na kuwa bora zaidi na hiki ndicho kipimo chake.
Aliwasihi wafanyabiashara hao kuwa na
maono ya mbali kutumia fursa za viwanda zinazokuja ikiwa ni pamoja na uwepo wa
chuo kikuu, chuo cha ufundi stadi, hospitali ya mkoa na kuwepo kwa migodi
mikubwa ambavyo vitachochea uchumi na biashara zao kukua
Hivi karibuni kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Songwe kiliazimia kwa
kupiga kura kuwa ofisi ya Mkuu wa mkoa huu ijengwe katika eneo la Nselewa na
idara nyingine za serikali zitatawanywa katika maeneo mbalimbali ya wilaya ya
Mbozi, hata hivyo uamuzi huo umeonekana kutokubaliwa na wakazi wengi wa Vwawa
kutokana na sababu mbalimbali.Mwisho
No comments:
Post a Comment