– Mbozi
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge
amezitaka mamlaka za maji kote nchini kuhakikisha zinatia dawa ya kutibu maji
kabla ya kuyasambaza kwa wananchi ili kujiridhisha kuwa maji yanayosambazwa ni
safi na salama.
Agizo hilo alilitoa
mwishoni mwa wiki wakati akiongea na wataalamu wa sekta ya maji mkoani Songwe
wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili kuwa hivi sasa serikali imeondoa
kodi ya ongezeko la tamani kwenye dawa za kutibu maji hivyo gharama yake kupungua
na kuwa hapatakuwa na sababu yoyote ya kushindwa kutia dawa kwenye maji kabla
ya kuyasambaza kwa wananchi.
Lwenge alisema sambamba na kutibu maji amezitaka pia mamlaka
hizo kuhakikisha wakazi waliopo kwenye vyanzo vya maji wanapatiwa huduma hiyo
ili waweze kuwa na ari ya kuvitunza, badala ya kuwaacha wakiyaona tu maji
yakipelekwa maeneo mengine na wao wakihangaika hawana maji safi na salama.
“ si vizuri watu waliopo kwenye vyanz wakaachwa bila huduma
hata kama maji ni kidogo nao wafikiriwe kwani wakati huu tunayaona maji kidogo
ya mgawo lakini iwapo tusipotunza vyanzo na mazingira utafika wakati hata hayo
maji kidogo hatutayaona na hapo ndipo hali itakuwa mbaya zaidi,”alisema Waziri
Lwenge
Awali akiwasilisha taarifa ya mkoa mkuu wa mkoa wa Songwe
Luteni Mstaafu Chiku Galawa alisema mkoa unakabiliwa na upungufu wa lita 12
milioni za maji kila siku kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kukauka kwa
vyanzo vya maji, miundombinu michakavu na ukame wa muda mrefu.
Alisema mkoa umeweka mkakati wa kvuna maji ya mvua kwa
kuhakikisha kila anayetaka kujenga anaonesha namna atakavyovuna maji na kuwa
utekelezaji wa mkakati huo umeanza katika taasisi za umma ili kuwaonesha mfano
wananchi.
Kwa uande wake Kaimu Meneja wa Mamlaka ya maji Vwawa Akiba
Kibona alikiri kutokuwa na mitambo ya kusafisha maji na hivyo kutokuwa na maji
safi, hata hivyo alisema wamekuwa wakitia dawa ya kuua wadudu kabla ya
kuyasambaza kwa wananchi.
Alibainisha kuwa hivi sasa wmeandaa andiko la kuomba fedha
ili kujenga mtambo wa kusafisha maji kabla ya kuyapeleka kwa wananchi.
Mkazi wa Mlowo Evarine Kayange alitupia lawama mamlaka ya
maji kwa kushindwa kuwawekea huduma hiyo katika eneo lao ambako kuna chanzo cha
maji cha Lutumbi hali ambayo ilisababisha baadhi ya watu kukata bomba ili nao
wapate huduma hiyo.
Aidha aliiomba serikali kuweka alama katika maeneo ambayo
hayastahili kufanyika shughuli za kibinadamu ili kuondokana na migogoro na
watendaji kwakuwa wananchi wengi wanashindwa kuelewa wapi hawastahili kufika.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment