Social Icons

Monday, 9 January 2017

Kizimbani Kwa Kuchoma Nyumba Moto na Kujeruhi



Stephano Simbeye,Mbozi: 

Wakazi watatu wa kijiji cha Ipanzya kata ya Ipunga wilayani Mbozi mkoani Songwe jana walipandishwa kizimbani katika mahakama ya wilaya ya Mbozi kujibu shitaka la kuchoma moto nyumba yenye thamani ya Sh. 1.2 milioni mali ya Wastafily Mwamlima kinyume na kifungu cha sheria namba 329 kanuni ya adhabu sura ya 16.

Ilidaiwa mahakamani hapo na mwendesha mashitaka wa polisi Diventini Nyahoro kuwa tukio hilo lilitokea septemba 11 mwaka jana saa 7 usiku, washitakiwa hao walivamia nyumba na kuichoma moto na kumjeruhi mwenye nyumba kwa makusudi bila halali huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Aliwataja Washitakiwa hao kuwa ni Obedi Luoga (51) ,Mwashuma Mwamlima (47) , Salum Abdala (32) wote wakiwa wakazi wa kijiji hicho

Aidha Nyahoro aliongeza kuwa nyumba hiyo yenye thamani ya sh. milioni moja na laki mbili iliyochomwa na washitakiwa hao na kumjeruhi mlalamikaji sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kutumia kisu huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Hata hivyo washitakiwa wote walikana shitaka hilo mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Nemes Chami  ambaye pia aliahirisha shauri hilo mpaka January 17 mwaka huu na washitakiwa wote wameachiwa kwa dhamana, kwa sharti la kuwa na wdhamini wawili kila mmoja na mali isiyohamishika.
Mwisho



No comments:

Post a Comment