Social Icons

Tuesday, 31 January 2017

Mpango wa Huduma ya Pamoja katika Mpaka wa Tanzania na Zambia Wasainiwa



Stephano Simbeye, Mbozi,

VWAWA: Serekali ya Tanzania na Zambia zimesaini mkataba wa makubaliano ya kuanzisha kituo cha pamoja cha  mpakani Tunduma na Nakonde nchini Zambia kwa lengo la kupunguza urasimu mpakani na kurahisisha ufanyaji biashara n a upitishaji wa mizigo mpakani.

 Akizungumza mara baada ya zoezi la kuweka saini Naibu Katibu mkuu  Wizara ya Fedha na Mipango Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Amina Shaaban alisema kukamilika kwa mpango huo ni utekelezaji wa agizo la marais  Dr. John Pombe Magufuli na rais Dr. Edgar Lungu wa Zambia alipofanya ziara hapa nchini ambapo walikubaliana kituo hicho mkianze kufanya kazi mara moja.

Alisema katika kufanikisha makubaliano hayo yametiwa saini na Makatibu Wakuu wa nchi hizi mbili wakiwa ni Makatibu wakuu wa Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya viwanda na uwekezaji wa Tanzania na Makatibu Wakuu wa wizara za biashara na viwanda, maendeleo ya nyumba na miundombinu na Jimbo la Mchinga wa Zambia ambao walikutana katika kikao cha pamoja kilichofanyika mjini Vwawa wilayani Mbozi mkoani Songwe.

Shaaban alisema pamoja na makubaliano ya kuanza kufanya kazi kwa kituo cha pamoja cha Tunduma/Nakonde, viongozi hao pia wamesaini mwongozo wa utendaji pamoja na mfumo  wa urahisishaji biashara kati ya nchi hizo mbili.   0763274634

Alisema hiki kitakuwa ni kituo cha tano kwa upande wa Tanzania ambapo vituo vingine ni pamoja na Holili-Taveta katika mpaka wa Tanzania na Kenya, Rusumo (Tanzania na Ruanda), Mutukula (Tanzania na Uganda), na Kabanga/Kobela (Tanzania na Burundi).

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Uwekezaji wa Tanzania Prof. Adol Mkenda alisema kusainiwa kwa mkataba huo kutasaidia kurahisisha ufanyaji biashara mpakani kwa bidhaa zile zinazotambuliwa pande zote bila usumbufu naMpango kumaliza biashara za magendo mpakani.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara wa Jamhuri ya Zambia Kayula Siame alisema maubaliano hayo yanafungua  ukurasa mpya wa ushirikiano kwa kuwa shughuli katika kituo zitafanyika kwa uwazi katika kituo kimoja.

Aidha alisema makubaliano hayo yatasaidia kuongeza mapato kwa pande zote na kukomesha biashara ya magendo ambayo inapoteza mapato ya serikali zote mbili na pia kuhatarisha usalama mpakani.

Aliongeza kuwa hiki kitakuwa kituo cha pili cha mpakani kikitanguiwa na kile cha Chilundu katika mpaka wa Tanzania na Zimbabwe.

Naibu Kamishina wa Mamlaka ya mapato Tanzania Charles Kicheele alisema ofisi yake imejiandaa kikamilifu kuanza kwa shughuli za pamoja mpakani ambapo kwa sasa wamekarabati jingo lililopo ili kuanza kazi mapema wiki ya kwanza ya mwezi Februari mwaka huu wakati kazi ya ujenzi wa jingo jipya ikiendelea.
Mwisho.



    

No comments:

Post a Comment