Social Icons

Saturday, 4 February 2017

Maduka Sita Yateketea Tunduma

Stephano Simbeye, Mwananchi
TUNDUMA: Maduka sita yameteketea kwa moto katika soko la Manzese katika halmashauri ya mji wa Tunduma wilayani Momba mkoani Songwe kutokana na hitilafu ya umeme na kusababisha hasara kubwa.

Mmoja ya wamiliki wa maduka jirani na yaliyoungua Itika Mwashibanda akizungumza kwa njia ya simu na mwandishi wa habari hizi alisema kwamba moto huo ulianza kuwaka saa sita usiku wa kuamkia leo ambapo unasadikiwa kuwa chanzo chake ni hitirafu ya umeme

Alisema hata hivyo kutokana na jitihada za wananchi kwa kushirikiana na jeshi la polisi na kikosi cha zimamoto cha Nakonde Zambia walifanikiwa kuuzima moto huo.

Geradi Donard ni shuhuda aliyekuwepo wakati moto huo unazimwa alisema chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umemeambapo umekuwa ukikatwa mara kwa mara na kurejeshwa kutokana na kuhamisha nguzo za umeme ili kupisha upanuzi wa barabara unaoendelea katika mji huo.

Alisema hili ni tukio la pili la kuteketea kw maduka ya wafanybiashara ambapo tukio kama hilo lilitokea maka jana na kuteketeza maduka matatu, hata hivyo wamekuwa wakipata msaada toka kikosi ch zimamoto kutoka nchi jirani ya Zambia na kuuzima moto huo.

Kamanda wa Polisi mkoani Songwe Mathias Nyange amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba uchunguzi bado unaendelea ili kubaini chanzo cha moto huo na pia bado thamani halisi ya mali zilizoteketea haijafahamika na hakuna madhara kwa binadamu.

Kamanda nyange ametowa wito kwa wafanyabiashara kote mkoani Songwe kuzima vifaa vyote vya umeme wanapofunga maduka yao ili kuepusha hitilafu inayoweza kutokea.
Mwisho

No comments:

Post a Comment