Stephano Simbeye, Mwananchi
Wajumbe wa Baraza la Mamlaka ya Mji mdogo wa Vwawa wilayani
Mbozi mkoa wa Songwe jana wameridhia kwa kauli moja kuunganisha mji huo na mji
wa Mlowo na miji mingine ili kukidhi vigezo vya kuunda Manispaa kwa sharti la kubadili jina.
Hayo yametokea jana katika kikao cha Baraza kilichofanyika
katika ukumbi wa Mamlaka hiyo mjini Vwawa mara
baada ya Ofisa mtendaji wa Mamlaka Joel Kaminyoge kutoa ufafanuzi wa ajenda hiyo akieleza faida
za kuundwa Manispaa kuwa ni pamoja na kupata miradi mikubwa ya maendeleo.
Alisema kwa muda mrefu mamlaka hiyo imekuwa ikijitahidi ili
ipande hadhi ili kufikia adhima yake ya kuwa halmashauri na kuboresha huduma
kwa wananchi wake.
Hata hivyo makubaliano hayo yalifikiwa kwa tabu kufuatia
wajumbe kupinga wazo la kuungana na Mlowo kwa madai kwamba huko nyuma waliwahi
kuomba waunganishe miji hiyo miwili lakini wenzao wa Mlowo walikataa na kuhoji
kulikoni leo huku wakilihusianisha jambo hilo na uamuzi wa eneo la kujenga
ofisi ya mkuu wa mkoa ambalo kiuhalisia wajumbe hao hawakubaliani na maamuzi
yaliyotolewa.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Vwawa sekondari Damasi Mlungu
alisema kuwa zaidi ya mara moja waliwafuata wenzao wa mji wa Mlowo ili kuungana
na kuunda halmashauri ya mji lakini waliwakatalia kwa madai ya kutoungana na
mji usiokuwa na mapato ya kutosha, kisha akahoji imekuwaje leo wanataka
kuwaunganisha kwa haraka.
“ tunatambua kuwa chanzo cha jambo hili ni makao makuu ya
mkoa baada ya kuona uamuzi umetolewa ofisi hizo zijengwe kwenye eneo lao sasa
wanaona umuhimu wa kuunganisha miji hii, sasa sisi tunakataa bali tuendelee
kupambana wenyewe ili kufikia vigezo stahili badala ya kuungana na hao” alisema
Mlungu.
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha Ilolo Ambakisye kibona
alisema kwa kuwa wakazi wa Vwawa wamedharaulika hawataweza kuungana na mlowo
kwa wakati huu.
Hata hivyo kufuatia wajumbe kuendelea kukataa kuridhia
kuunganisha miji hiyo miwili ili kupata Manisaa moja Mbunge wa jimbo la Vwawa
Japhet Hasunga alitowa ufafanuzi na uelewa kwa wajumbe kuwataka kuunga mkono
wazo lililopelekwa mbele yao.
Alieleza faida za
kuwa na Manispaa kwa maendeleo yao kuwa ni pamoja na bajeti kuongezeka ili
kupata maendeleo ya haraka na miradi mikubwa ya Benki ya dunia ya kuboresha
miundombinu ya barabara na huduma nyingine nyingi za kijamii.
Aidha Hasunga aliwasihi wajumbe kukubaliana kuungana ili
kutimiza vigezo vya kuunda Manispaa hiyo ambayo ni kwa ajili yao na kuwa ofisi
zake zitawekwa katika eneo lao kwa ajili ya manufaa ya wakazi wa eneo hilo na
si vinginevyo.
Naye mkuu wa wilaya ya Mbozi John Palingo aliwasihi wajumbe
hao kuacha kuhusianisha ofisi za mkuu wa mkoa na uanzishaji wa manispaa na
kwamba Manispaa ni yao, ndiyo yenye faida kwao ukiinganisa na ofisi ya mkuu wa
mkoa
“Nashauri tukubali kuunda Manispaa ndiyo italeta maendeleo
ikiwemo miradi mikubwa, lakini pia nashauri mtulie pamoja na kuwa muna hasira
kutokan*--a na michakato mingi imekosewa na ndiyo chanzo chanzo cha hasira za
wajumbe , lengo la kasi hii ni zuri ili kwenda na kasi ya wenzetu waliko mbali”
alisema Mkuu huyo wa wilaya.
Kufuatia ufafanuzi uliotolewa na viongozi hao mwenyekiti wa
Mamlaka hiyo Ephraim Mwakateba aliwahoji wajumbe wake kama wanakubaliana kuunda
Manspaa ndipo walikubali kwa sharti la kutaka kubadili jina badala ya kuitwa
Manispaa ya Mbozi iitwe manispaa ya Vwawa.
Aidha hasira za wajumbe hao zinatokana na kubadilishwa eneo
la kujenga ofisi za mkuu wa mkoa, ambapo awali ilipendekezwa zijengwe katika
mojawapo kati ya maeneo matatu ya oldvwawa, TacRi Mbimba na Hasamba yaliyopo
kata ya Vwawa, lakini tofauti na hilo hivi sasa uamuzi umetolewa kuwa ofisi
hizo zijengwe eneo jipya la Nselewa lililopo kata ya mlowo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment