Social Icons

Saturday, 14 January 2017

Stephano Simbeye, Mbozi



Wafanyabiashara na wadau mbali mbali wa elimu wilayani mbozi mkoani Songwe wameombwa kutoa misada katika shule zilizopo wilayani hapa ili kuipunguzia mzigo serikali kwani haiwezi peke yake kumaliza changamoto zilizopo katika jamii.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbozi Edna Mwaigomole wakati akipokea fulemu tano zenye thamani ya zaidi ya sh. Laki 5 za shule ya msingi Nuru iliopo vwawa wilayani hapa kutoka kwa mdau wa elimu Exaud Kajela.

Mwaigomole ameongeza kuwa msaada ambao umetolewa na mdau huyo utasidia kupunguza changamoto zinazoikabili shule ya nuru ambayo ni mpya na haina milango wa fulemu za madirisha.

Akizungumza wakati akikabidhi msaada huo Exaud Kajela amesema kuwa amesukumwa kuchangia fulemu hizo baada ya kupata taarifa kutoka kwa mwalimu kuwa kuna changamoto wakati wa kufundisha wakati mvua zikinyesha hivyo uelewa kwa wananfunzi unakuwa tatizo kubwa.

Kwa upande wake afisa elimu ufundi wilayani Mbozi Nobati Kisimba kuna uhitaji wa madarasa 2242 lakini vilivyopo ni 1228 kwa iyo kuna upungufu wa madarasa 967 na upungufu utazibwa na shule 10 zinazojengwa wilayani hapa na tano kati ya hizo zitakazokamilika mapema zitaanza mwaka huu.

Naye mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nuru Fausta Nzunda akitoa maelezo ya awali katika hafla hiyo alisema shule hiyo ilianza mwaka 2013 ikiwa ni mchepuo kutoka shule mama ya Haloli baada ya kufulika wanafunzi, imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya vyumba vya madarasa hali inayofanya wanafunzi warundikane katika vyumba vichache vilivyopo na hivyo kutosoma vizuri.

Kufuatia changamoto hiyo wananchi waliamua kujenga vyumba vitatu vya madarasa tangu mwaka 2014 kwa gharama ya Sh.3.09milioni, nayo halmashauri ya wilaya ya Mbozi ilitoawa Sh. 4.03milioni ili kuunga mkono jitihada za wananchi, ofisi ya Mbunge wa jimbo la Vwawa ilitowa 2.150milioni hata hivyo majengo hayo bado hayajakamilika hali iliyofanya waanze kutafuta wadau wa kusaidia na ndipo walipompata Exaudi Kajela.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment