Social Icons

Friday, 24 February 2017

CWT YAANZA KUHAMASISHA MICHEZO KWA WALIMU

Stephano Simbeye,
 
Vwawa:
Chama cha walimu Tanzania (CWT) kimeanza kugawa mipira ya michezo mbalimbali mashuleni kwa ajili ya kuhamasisha walimu kuunda timu ikiwa ni hatua ya kuhamasisha wafanye mazoezi ili kuboresha afya zao.
 
Katibu wa chama hicho wilayani hapa Herbet Mkonjera akiongea wakati wa hafla fupi ya kukabidhi mipira 60 jana kwa ajili ya walimu wa shule za msingi na sekondari alisema kuwa mipira hiyo imetolewa na Naibu Katibu mkuu wa CWT Taifa Ezekiel Ouloch kwa lengo la kuwafanya walimu waunde timu zao za michezo mbalimbali ambayo itakuwa ni hatua ya kuunga mkono agizo la Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan la kuwataka watanzania kufanya mazoezi.
 
Aliwataka walimu kupanga ratiba ya mazoezi na ikibidi kuwa na mashindano na shule nyingine, ama na waratibu ambao nao wamepatiwa mipira yao ili waunde timu yao.
 
Akizungumza kabla ya kukabidhi mipira hiyo Mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya mbozi George Mwakapala alisema zoezi la kutoa mipira kwa walimu litakuwa endelevu kila mwaka na kuwa chama hicho kinakusudia kuunda timu moja ya wilaya ambayo itatokana miongoni mwa wachezaji watakaokuwa kwenye timu za shule.
 
‘tunataka mwisho wa siku timu ya wilaya tuipandishe daraja hadi icheze ligi kuu tokea mkoa wa Songwe,  hata hivyo CWT haikuangalia mpira wa miguu tu bali ni pamoja na mpira wa mikono na pete pia“alisema Mwenyekiti huyo
 
Mmoja wa wawakilishi wa walimu Victoria Kibona alisema mipira hiyo itatumika kwa ajili ya michezo ya walimu tu kuimarisha afya zao na kuwa pia kitendo cha walimu kuanza kucheza pia kitachochea michezo kwa wanafunzi nao kuanza kuibua vipaji vyao
 
 Sadrick Mwashilindi ni mjumbe wa CWT wilaya anayewakilisha kundi la vijana alisema kupitia michezo kutawaweka walimu katila mshikamano zaidi na hivyo kutimiza lengo la kuanzishwa kwake la kiws na sauti moja
Mwisho

No comments:

Post a Comment