Stephano Simbeye, Mbozi
Mvutano wa eneo la kujenga ofisi ya mkuu wa
mkoa wa Songwe umeingia katika sura mpya baada ya jumuia ya
wafanyabiashara mjini Vwawa kukihoji chama cha Mapinduzi kwa kushindwa kutolea
tamko suala la eneo la kujengwa ofisi za mkuu wa mkoa badala ya Vwawa ilikoamliwa awali na kupelekwa Selewa
Mwenyekiti wa Jukwaa la wafanyabiashara
Yohana Mwajeka Akitoa utangulizi katika kikao kilichofanyika katika ukumbi
wa Moravian Vwawa mjini wilayani Mbozi mkoani hapa alisema mchakato
ulipokamilika wa kuanzishwa mkoa wa
Songwe lilitolewa tamko na viongozi wa
juu wa serikali ya awamu ya nne kuwa makao makuu yatakuwa kata ya Vwawa, pia
suala hilo lilinadiwa kama moja ya mambo yaliyotekelezwa na Mbunge aliyemaliza
muda wake Godfrey Zambi ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya.
Alisema kinachowafanya wahoji suala hilo ni
kutokana na mabadiliko yaliyotokea ya kubadilisha eneo la kujenga ofisi za mkuu
wa mkoa badala ya kata ya Vwawa yamepelekwa Selewa iliyopo kata ya Mlowo jambo
ambalo wao wanaona ni ukiukwaji wa matamko ya viongozi wa juu.
Edward Mahenge (Ndisana) alisoma bango
lililoandikwa na Mbunge aliyemaliza muda wake Godfrey Zambi likieleza
utekelezaji wa Ilani ya CCM kuwa eneo la Vwawa amefanikiwa kuanzisha mkoa mpya wa Songwe na makao makuu yatakuwa Vwawa.
"Tulipoambiwa hapa patakuwa makao
makuu tulijiandaa kutumia fursa hiyo kuwekeza, sasa tunakohoji Mwenyekiti kuwa
chama kilitudanganya, kama sivyo nani kabadilisha tamko lililotolewa na
Rais" alihoji Mahenge
Isaya Mwakidodi alisema Rais John Magufuli wakati wa
kampeni za uchaguzi mwaka juzi aliwaahidi wanavwawa kuwa mkoa mpya unaanzishwa
na kuwa makao makuu yatakuwa Vwawa na pia aliahidi kutengeneza barabara yenye urefu
wa kilometa kumi kwa kiwango cha lami lakini wanaona kauli ya Rais na
Waziri mkuu Mmstafu Mizengo Pinda
zimebadilishwa huku chama kikiwa kimywa.
Akijibu hoja za wafanyabiashara hao
Mwenyekiti wa Chama cha Mapindizi wilaya ya Mbozi Aloyce Mdalavuma alikiri
kuwapo na kauli za ahadi za viongozi wakuu wa nchi kama Waziri Mkuu mstaafu
Mizengo Pinda na Rais John Pombe Magufuli alitoa ahadi ya Vwawa kujengwa ofisi
ya mkuu wa mkoa na kwamba chama hakiwezi kuwa tofauti na Mwenyekiti wake wa
taifa.
Alisema chama cha Mapinduzi wilayani Mbozi
kilishiriki katika uanzishaji mkoa wa Songwe na kushiriki mapendekezo ya maeneo
matatu ya Oldvwawa, Mbimba na Ilembo/Hasamba lakini eneo la nne laSelewa hakikushiriki.
Sakata la mgogoro wa kugombea eneo la
kujenga ofisi za mkuu wa mkoa wa Songwe lilianza mwishoni mwa mwezi Desemba
mwaka jana mara baada ya kamati ya ushauri mkoa (RCC) kuazimia ofisi hizo kujengwa eneo la Selewa
lililopo kata ya Mlowo, badala ya kata Vwawa kama ilivyoahidiwa wakati wa
mchakato.
Tayari makundi mbalimbali yameanza harakati
za kugombania maeneo haya ambapo wiki iliyopita wafanyabiashara na wadau wa mji
wa Mlowo walikutana katika kikao ambapo waliazimia kuunda kamati ya watu 15
ambao watafuatilia kuona pendekezo la ofisi za mkoa kujengwa Selewa yanabaki
kama yalivyo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment