Social Icons

Thursday, 23 March 2017

Amchaanga na Mapanga mkewe kisa Nyama

Na: Stephano Simbeye



ILEJE: Mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha Igumila wilayani Ileje mkoani Songwe Yeska Mlungu (50) amejeruhiwa vibaya baada ya kukatwa mapanga na mume wake kwa madai ya kutompakulia nyama aliyoinunua.

Shuhuda mmoja ambaye pia ni jirani wa familia hiyo Lukas Swila alisema wa tukio hilo lilitokea juzi ambapo walisikia kelele za mama huyo kuomba msaada na walipofika walikuta amepoteza fahamu huku akitokwa na damu nyingi kutokana na majeraha aliyokuwa nayo.

Alisema baada  ya hapo kwa kushirikiana na majirani wengine waliitaarifu polisi ambao walitowa fomu ya matubabu (PF3)  na kwenda hadi kwenye hospitali ya wilaya ya Ileje (Itumba).

Akielezea tukio hilo Mama huyo katika hospitali ya Itumba alisema chanzo cha ugomvi wao ni nyama ambao mume wake huyo aitwaye aliinunua, lakini kutokana na kuwa ilikuwa kidogo aliwapakulia watoto na mume kukosa

Mganga wa zamu  wa hosptali ya Itumba Samsoni Wangwi  alisema alimpokea  majeruhi huyo  akiwa na hali mbaya iliyotokana na kuvuja damu nyingi kutokana na kupata majeraha makubwa.

Naye kaimu mganga mfawidhai wa hosptali ya Itumba Damas Banzi alisema kuwa baada ya kuanzishiwa matibabu hali ya majeruhi inaendelea vizuri na kwamba  mwanaume huyo kitendo alichofanya ni ukatili ambao unatakiwa kupigwa vita na elimu kutolewa kwa wanaume wenye tabia kama hiyo.

Banzi aliongeza kuwa kwa sasa wanajitahidi kumpatia matibabu mama huo ili kuurudisha mwili wake katika hali yake ya kawaida licha ya kuwa amejeruhiwa vibaya.

Kamanda wa polisi mkoani Songwe,Mathias Nyange,alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa ametorokea kusiko julikana baada ya kutenda tukio hilo jana saa mbili usiku na jeshi lake linaendelea kumsaka.

Aliongeza kuwa mashirika binafsi na jamii kwa ujumla inatakiwa kushirikiana ili kupiga  vita vitendo hivyo na kusema kuwa wao kama jeshi la polisi watasimama kidete kupinga vitendo hivyo na kuwafikisha  kwenye mikono ya sheria  wale wote ambao  wanawapiga na kuwanyanyasa wa wanawake.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment