Social Icons

Thursday, 23 March 2017

Kabui la Albino Lafukuliwa

Na: Stephano Simbeye



WATU wasiofahamika wamefukua kaburi la mlemavu wa ngozi [ALBINO] kisha kuchukua mifupa  na kubakiza fuvu la kichwa na kutokomea kusikojulikana, katika kijiji cha Nansama kata ya Isansa wilayani Mbozi mkoani Songwe.

Akisimulia mkasa huo jana, shemeji wa marehemu Sala Kamwela, alisema shemeji yake alifariki Marchi 28 mwaka 2011 akiwa na umri wa miaka 50 ambapo jana alisema alishangazwa kuona kaburi lake lililosakafiwa na saruji lilikutwa limefukuliwa na kuondolewa mifupa wakibakiza fuvu la kichwa.

Alisema baada ya tukio hilo,ambalo waliligundua wakati wanarudi kutoka shamba,wakalazimika kutoa taarifa kwa Mwenyekiti wa kitongoji na kijiji na hatimaye polisi kwa kushirikiana na serikari ya kijiji ambayo ilifika eneo la tukio wakiwa na daktari na mara baada ya uchunguzi walizika upya fuvu hilo na masalia mengine.

Akizungumzia tukio hilo mjumbe wa kamati ya kijiji,Baraka Ntenga,alisema marehemu alikuwa ndugu yake anasikitika kuona kaburi limefukuliwa na kuwa anaomba jeshi la polisi liwasake waliohusika kufukua kaburi hilo.

Alisema tukio hilo ni la kwanza kutokea katika  kijiji chao na  kuwarudisha nyuma kipindi cha matukio ya uchunaji ngozi za binadamu ulioshamili wilayani mbozi ambayo yalihusishwa na imani za kishirikina,kwa sasa yametoweka .

Kamanda wa polisi mkoani Songwe,Mathias Nyange amthibitisha kutokea tukio hilo,na kusema limetokea usiku wa kuamkia jana na kuwa jeshi lake linaendelea kuwasaka waliohusika na tukio hilo.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoani humo,Luteni mtaafu, Chiku galawa,alisema vitendo hivyo vinapaswa kukemewa kwa nguvu zote kutokana na kuhusishwa na imani za kishirikina na kuwa ikiwa wanafukuwa makaburi wataweza kuwafuata walio hai na kuwaangamiza.

Galawa ambaye pia ni mkuu wa mkoa huo, alisema atawasiliana na machifu na viongozi wa dini zote kushirikiana na serikali kupiga vita matukio hayo yanayohusishwa na imani za kishrikina.
Mwisho.


No comments:

Post a Comment