Social Icons

Wednesday, 15 March 2017

DC, Awataka Watumishi wa Serikali Kufuata Sheria za Usalama Barabarani



Stephano Simbeye, Mwananchi
ssimbeye@mwananchi.co.tz

Tunduma: Mkuu wa wilaya ya Momba Mkoani Songwe Juma Erando amewataka watumishi wa serikali wanaomiliki vyombo vya moto kuingia darasani kusomea udereva ili wapate uhalali wa kuendesha vyombo hivyo.

Kauli hiyo aliitowa Jana katika siku ya hitimisho ya mafunzo ya waendesha pikipiki alimaarufu (boda boda) Yaliyo fanyika Mji wa Tunduma uliopo wilaya ya Momba Mkoani Songwe.

Alisema kumekuwa na watumishi wengi wa Serikali wanao miliki magari yao na kuyaendesha pasipo na mafunzo yoyote na kuwa kufanya hivyo inaweza ikawa chanzo cha ajari zinazo tokea Barabarani kila siku.

Juma aliwasistiza wahitimu wanao maliza mafunzo ya udereva pikipiki (Boda boda) kuto kuvunja sheria zirizo wekwa pamoja na maandamano au kutumika kisiasa. Pia katika hitimisho la mafunzo hayo Mratibu na mkufunzi wa mafunzo ya usalama Barabarani kutoka Shirika lisilo la kiserikari APEC Peter John Peter.

Ameiomba Serikali kuwapatia wahitimu wa mafunzo hayo bima ya afya pamoja na kuwapatia Leseni mapema bila vikwazo vyovyote. Mwisho
Mwisho.

No comments:

Post a Comment