Social Icons

Wednesday, 1 March 2017

Polisi Wanasa Mashamba ya Bangi





Stephano Simbeye, 

Jeshi la Polisi mkoani Songwe linawashikiria watu sita (6) wakazi wa wilaya tatu za Mbozi, Ileje na Momba mkoani Songwe, baada ya kukutwa wamelima bangi katika  mashamba yeknye ukubwa wa hekari 10.1/2 wakiwa wamechanganya katika mashamba yao waliyolima zao la mahindi kinyume cha sheria.

Kamanda wa polisi mkoani hapa Mathiasi Nyange alisema watu hao walikamatwa katika msako wa matumizi ya dawa za kulevya unaoendelea nchini kote ambapo jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata watu wawili wenye umri wa miaka 41 na 53 (majina yamehifadiwa)  wakazi wa kijiji cha Shaji kata ya Mlangali wilayani Mbozi akiwemo Mwenyekiti wa kitongoji, wakiwa wamepanda bangi katika shamba lenye ukubwa wa hekari tano huku ndani yake likiwa limechanganywa na mahindi.

Alisema katika tukio lingine katika kijiji cha Zelezeta kata ya Igamba wilayani Mbozi mtu mmoja mwenye umri wa miaka 35 alikamatwa akiwa anamiliki shamba lenye ukubwa wa hekari 2 na Iyua robo eari, wakati huko katika wilaya ya Ileje katika kijiji cha Mbebe mtu mmoja alikutwa na shamba lenye ukubwa wa nusu hekari na katika kijiji cha Chipaka wilayani Momba mtu mmoja alikutwa na shamba lililopandwa bangi hekari mbili na nusu.

Nyange alisema  watuhumiwa hao wanatarajia kufikishwa mahakamani wakati wowote na msako dhidi ya walima bangi ni endelevu hadi watakapohakikisha hakuna tena ulimaji wa zao hilo mkoani hapa, pia ametahadharisha viongozi wa vijiji ambao wanafumbia macho walimaji wa bangi ambapo ameapa kuwachukulia hatua za kisheria.

Mwenyekiti wa kijiji cha Shaji Goodwell Haonga akizungumzia tukio la mkazi wa kijiji hicho kukutwa na shamba la bangi alisema anashangazwa na hali hiyo kwani mwanakijiji huyo makazi na mashamba yake viko pembeni kidogo na makazi yaw engine hivyo inakuwa vigumu kuona na kutambua hali hiyo.

Mkuu wa wilaya ya Mbozi John Palingo akizungumzia operesheni hiyo alionya watu wanaolima bangi waache kufanya hivyo kwani mkono wa serikali ni mrefu utawabana na watajikuta pabaya na badala yake walime mazao yanayokubalika.
mwisho

No comments:

Post a Comment