Stephano Simbeye, Mbozi
SAKATA la kuondolewa dhamana, Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Mbozi mkoani Songwe
madiwani 20 kati ya 39 wa halmashauri hiyo,wamesusia vikao vilivyofanyika April 20 na 21 mwaka huu na kutoka nje
ya ukumbi kwa madai ya kupinga mwenyekiti anayeongoza vikao hivyo Erick
Ambakisye uenyekiti wake uliondolewa dhamana na kamati ya siasa ya CCM kwa kushindwa
kuisimamia halmashauri na kusababisha upotevu wa Sh. 410milioni na kupatikana
kwa hati za mashaka miaka minne mfululizo ndani ya uongozi wake.
Ambakisye aliondolewa udhamini na Chama Cha Mapinduzi
(CCM) April mosi mwaka huu, hivyo kukosa
sifa za kuwa mwenyekiti na kupelekea madiwani 15 wa UKAWA na wa 5 wa CCM kutoka
nje ya ukumbi wakidai mwenyekiti huyo hana sifa ya uenyekiti huku madiwani 19
wakiendelea na kikao cha kupitisha taarifa za kata na baraza kamili cha April
21 mwaka huu.
Akizungumza mara baada ya kutoka nje ya
ukumbi,mwenyekiti wa kambi ya upinzani Maarifa Mwashitete,alisema mapema mwezi April
mwaka huu chama hicho kupitia Katibu wake Kaimu Katibu George Silindu kilitoa
tamko mbele ya waandishi wa habari kuhusiana na hatua iliyochukuliwa na Kamati
ya Siasa wilayani hapa na kuwasilisha barua kwa Mkurugenzi Mtendaji wa
halmashauri kwa ajili ya hatua zaidi za kumsimamisha uongozi na kumtaja makamu
Mwenyekiti wa halmashauri Alan Mgula kukaimu nafasi hiyo.
Alisema kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania ni kuwa diwani anapatikana kupitia chama cha Siasa, hivyo kama
chama chake kikiondoa dhmana anakosa sifa ya kuwa diwani kama ilivyofanyika kwa
kamati ya siasa ya CCM kuondoa dhamana kwa mwenyekiti huyo.
Alisema chanzo cha Mwenyekiti huyo kuondolewa
ni kushindwa kuwajibika na kuisababishia halmashauri hiyo kupata hati zenye
mashaka kwa miaka minne mfurulizo na kibaya zaidi alisema mwenyekiti
huyo,amesababisha ubadhirifu wa fedha million 410 pamoja na milioni 70 za
ujenzi wa ghala la Mlowo.
Alisema serikali ilitoa milioni 70 kwa ajili ya
ujenzi wa ghala hilo lakini ujenzi haujafanyika na fedha hazionekani na kwamba
mbali na hilo kuna ubadhirifu mwingi katika ujenzi wa miradi mingine hali
inayopelekea mwenyekiti huo kushindwa kusimamia majukumu yake ya kazi hivyo
alisema hawapo tayari kufanya nae kazi.
Naye Katibu wa madiwani wa CCM katika
halmashauri hiyo,George Msyani alikiri kuwepo na tuhuma hizo na kusema kuwa
yeye ni mjumbe wa kamati ya Siasa na diwani kata ya Nanyala alikuwepo katika
harakati za kumvua udhamini mwenyekiti huyo kutokana na kuwepo kwa tuhuma
lukuki za ubadhirifu.
Alisema baada ya kupeleka muhtasari wa kuondoa
udhamini kwa mwenyekiti huyo,kwa mkurugenzi,mkurugenzi aliwapa kanuni za
taratibu za kumvua uenyekiti ambayo inakinzana na kanuni iliyotumika kwenye
kamati ya siasa hivyo wanatakiwa kujipanga upya.
Aliongeza kuwa licha ya kuwepo kwa tuhuma za
ubadhirifu katika halmashauri hiyo,lakini kumekuwepo kwa vita ya kisiasa ambayo
baadhi ya vigogo wanadhani mwenyekiti huyo anajipanga kugombea Ubunge 2020.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye
pia ni diwani kata ya Bara Aloyce Mdalavuma alisema kamati ya siasa imeondoa
udhamini kwa mwenyekiti huyo lakini walipopeleka barua kwa Mkurugenzi
ilionekana kanuni ya halmashauri inakinzana na kanuni waliyoitumia.
Alisema suala hilo linasubiri uamuzi mwingine
wa chama na kuwa iwapo maamuzi mengine yatatolewa wananchi watajulishwa lakini
kwa wakati huu waendelee kusubiri
‘’Ni
kweli wananchi wamekosa imani na utendaji wetu katika halmashauri hii,kupata
hati nne mbaya inatukosesha amani kwa wananchi” alisema Mdalavuma.
Kwa Upande wake mwenyekiti Erick
Ambakisye,alisema njia iliyotumika kumuondolea udhamini haikufuata taratibu kwani kufuatia sakata hilo hakuna sehemu
alipoitwa kuhojiwa na ngazi yeyote ya chama na kuwa kutokana na mapungufu hayo
Mwenyekiti wa chama anapaswa aitishe mkutano na waandishi wa habari ili
kukanusha sintofahamu iliyojitokeza na kuwa hayo ndiyo makubaliano mapya
yaliyofikiwa.
Mwisho
No comments:
Post a Comment