Stephano Simbeye, ILEJE
Wafanyakazi mkoani Songwe,
wametakiwa kwa kwa malengo ambayo yataleta tija inayoonekana kwa wananchi ikiwa
ni pamoja na kuinua pato la mtu kutoka pato la sasa la Sh. 1.3 milioni na kuwa
zaidi ya Sh. 7 milioni za lengo la Taifa kwa mwaka.
Mkuu wa mkoa wa Songwe Chiku Galawa
alisema hayo jana wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani
iliyoadhimishwa kimkoa mjini Itumba wilayani Ileje, kuwa kila mfanyakazi ni
lazima awe na mpangokazi ambao utasaidia kuleta mabadiliko ya kiuchumi kwa
walengwa badala ya kutoa taarifa za maneno ambazo hazisaidii kuinua maisha ya
watu.
Alitolea mfano kwa wataalamu wa
ugani kuwa wanaweza kuweka lengo la kumwezesha mkulima kuongeza
uzalishaji,mfano zao la mahindi kuwa hivi sasa wakulima wanapata gunia kati ya
8 na 15 kwa hekari moja hivyo anahitajika kuwezeshwa ili aongeze uzalishaji
hadi kufikia gunia 25 na 30 kwa hekari moja hali kadhalika katika sekta
nyingine zote zinapaswa kuwa hivyo.
“ acheni mtindo wa kufanya kazi kwa
mazoea timizeni wajibu wenu kwanza, mkifanikiwa kuongeza pato ndipo mdai haki
maana iwapo mtaongeza pato la mwajiri ni rahisi kwake kuwaongeza stahiki zenu”
alisema Galawa.
Awali katika risala ya wafanyakazi
iliyisomwa na katibu wa CWT mkoa wa Songwe Emelia Mwakyoma alisema wafanyakazi
wamekuwa wakifanyakazi kwa manung’uniko mengi yahusuyo upatikanaji wa stahiki
zao ikiwemo kutolipwa madeni muda mrefu pamoja na kufanyika kwa zoezi la
uhakiki.
Aidha Mwakyoma aliongeza kuwa suala
la kuongezwa kwa makato ya wanufaika wa bodi ya mikopo ya elimu ya juu toka
asilimia 8 hadi 15, imewaongezea wakati mgumu wa maisha watumishi kutokana na
kuwa wengi wao wanakabiliwa pia na makato yanayotokana na mikpo waliyokopa toka
taasisi za fedha na hivyo kufanya wasipate kitu chochote.
Mmoja wa wafanyakazi Edina Kalinga
alisema wafanyakazi wapo tayari kufanya kazi kwa bidii na kwa malengo ya hali
ya juu, lakini wamekuwa wakitatizwa na ukosefu wa vitendea kazi kama usafiri na
rasilimali fedha ili kuweza kufika waliko wananchi na badala yake wanalaimika
muda mwingi kuutumia wakiwa ofisini wakifanya kazi kwa kuagiza badala ya kufika
wao wenyewe.
Alisema tunaiomba serikali iweke
mazingira rahisi ikiwa ni pamoja na kuwapatia vitendea kazi kama usafiri ili
kuwarahisishia kutimiza majukumu yao, pia iongeze bajeti ya uendeshaji.
Mwisho
No comments:
Post a Comment