Stephano Simbeye,
MBOZI: Wakulima wa kikundi cha wakulima Ichenjezya Saccos
wilayani Mbozi mkoani Songwe, wameomba kupatiwa mafunzo kwanza, kabla ya kuanza
kulima na kupanda katika mashamba yao ili ujuzi wanaopata wautumie kwa vitendo
mashambani mwao.
Hayo yamesemwa leo katika kijiji cha Nselewa ambako wakulima
hao walikutana kwa ajili ya mafunzo katika shamba darasa ambapo walisema licha
ya kupatiwa mafunzo hayo lakini tayari sehemu kubwa wamekwishalima na kupanda
kwa mbinu walizozizowea jambo ambalo halijawasaidia sana.
Sekelo Kayange alisema kuanzia mwakani ni vizuri wakulima wa
kikundi hicho wakapatiwa mafunzo kwanza katika shamba darasa, kabla ya kupatiwa
pembejeo ndipo waendelee kuendeleza mashamba yao ili wataalamu wanapotoa
mafunzo ya namna ya kupanda kwa kutumia pembejeo za kisasa ili katika muda ule
ule waweze kutumia maarifa hayo kwenye mashamba yao ili kuleta tija.
“ wakulima wengi hawajachukulia suala la mafunzo kwa umuhimu
unaopaswa, hivyo wanapaswa
kujifunza kwanza ndipo hatua nyingine zifuate”
alisema Kayange.
Katibu wa kikundi cha Ichenjezya Joseph Masanja alisema wazo la kupatiwa mafunzo
mapema waliliona lakini walipowasiliana na watu wa makampuni ya Mbegu walidai
wasubiri mvua ziongezeke kwani kuanza kupanda katika mashamba darasa wakati
mvua ni chache zinaweza zisiote vizuri kutokana na ukame lakini wakulima
wakaona kama mbegu zao hazifai hazifai.
“ hii ni changamoto
kubwa maana kumfundisha mtu jinsi ya kupanda wakati alikwishap
anda haina maana
yoyote lakini na sisi tumeliona jambo hilo tutalifanyia kazi ili mwakani yawepo
marekebisho yatakayowasaidia wakulima ikibidi hata kumwagilia”alisema Masanja
Mtaalamu wa ugani aliyefika kuwafundisha wakulima hao
Bornwelo Nzunda alisema wakulima wanatakiwa kuzingatia mafunzo yanayotolewa
kupitia vikundi vyao kwa njia ya mashamba darasa kwani ni muhimu kufikisha
maarifa yaliyokusudiwa kwao yatakayowasaidia kuboresha kilimo na kuwafanya
waongeze tija.
Alieleza kusikitishwa na mahudhurio mabovu ya wakulima
kwenye mafunzo jambo ambalo alisema litawafanya waendelee kurudi nyuma
kiuzalishaji kwani kwa sasa ardhi inazidi kupungua huku watu wakiongezeka,
kinachohitajika hapo ni kulima kilimo cha kisasa ambacho kitasaidia kupata mazao
mengi katika eneo dogo.
Wiki iliyopita Mkuu wa mkoa Songwe Chiku Galawa akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake aliagiza wataalamu wa ugani kuondoka
ofisini na kuanzisha mashamba darasa katika maeneo yao ili wakulima wayatumie
kupata maarifa yatakayowasaidia kuboresha kilimo chao ili kuongeza tija na
kwamba hicho kitakuwa kipimo cha kila mgani.
Aidha Galawa alisema mkoa umeweka mkakati wa kuongeza
uzalishaji ikiwa ni pamoja na kudhibiti uingizaji wa pembejeo feki kwa
kuwatambua wasambazaji wa pembejeo kila eneo ambapo alisema mkoa unatarajia
kuongeza eneo la uzalishaji la hekta 299393 katika msimu wa kilimo 2017/2018
badala ya hekta 250117 zilizolimwa mwaka jana.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment