Social Icons

Wednesday, 27 February 2019

Matukio Katika Picha Ziara ya Waziri Mhagama Kituo cha Vijana Sasanda Mbozi


 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na vijana wanaopata mafunzo ya kilimo bora na ufugaji wa kisasa katika kituo cha Maendeleo ya Vijana – Sasanda kilichopo Kata ya Nyimbili, Mkoani Songwe alipofanya ziara kukagua maendeleo na miradi ya vijana katika kituo hicho.



 




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akioneshwa na kupata maelezo ya vifaa vinavyotumiwa na vijana wa kituo cha Sasanda katika shughuli ya kuvua samaki.
Bi. Oliveta Mwashilindi akimueleza jambo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama kuhusu bidhaa ya asali inayotengenezwa na kikundi cha vijana cha Maisha Daily kilichopata mafunzo ya ufugaji nyuki katika kituo cha Sasanda.

No comments:

Post a Comment