Social Icons

Thursday, 14 March 2019

Wafurahia Mbio Za Mwenge wa Uhuru Kuzinduliwa Mkoani Songwe





Na: Mwandishi wetu Mbozi:  
  
Baadhi ya wananchi wa mkoa wa Songwe wamesema wana matumaini ya kuboreshewa miundombinu ya barabara na fursa ya kufanya biashara katika kipindi cha uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka huu utakaofanyika April 2 mwaka huu.

 Mkazi wa kijiji cha Idiwili William Mwahalende alisema kwa kuwa hii ni mara ya kwanza tukio kama hilo kufanyika katika mkoa huu, ni vizuri Serikali ikaelekeza nguvu zake katika kuboresha miundombinu ya barabara  na madaraja ambazo nyingi hazipitiki katika kipindi hiki cha masika.

Mkazi  wa Vwawa Mbwiga Mwampashe alisema tukio hilo ni la kihistoria kwa wilaya ya Mbozi na mkoa wa Songwe kwa ujumla, hivyo wamejiandaa kuitumia fursa hiyo kufanya biashara hivyo kuongeza kipato chao kwa kuuza bidhaa mbalimbali ikiwemo vyakula.

Aidha mwampashe alisema kuwa serikali imewatendea mambo mema wana songwe ambapo kwa mwaka huu  wamepata waziri mwenye dhamana ya kilimo, kwa ujumla ni jambo la kushukuru mungu. 

Naye Mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoani hapa Yohana Mwajeka alisema wafanyabiashara wamejipanga kutumia nafasi hiyo kufanya biashara katika kipindi chote cha maandalizi ya uzinduzi wa Mwenge na hadi kufikia siku yenyewe.

Mkuu wa mkoa wa Songwe Brigedia Jeneral Nicodemus Mwangela akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana aliwaomba wananchi kushiriki katika tukio la uzinduzi wa mbio za Mwenge kitaifa kwa kuonyesha umoja, mshikamano na uzalendo, ambapo alisema hiyo ni fursa pekee ya kuutangaza mkoa na fursa zake za kiuchumi zilizopo.

Sambamba na fursa hizo pia alisema itakuwa ni mara ya kwanza mwenge kuwashwa katika mikoa ya nyanda za juu kusini husuani mikoa ya Mbey ,Songwe ,Iringa,Rukwa ,Njombe na Katavi kwa zaidi ya miaka 10 iliyo pita.

Aidha mkuu huyo wa mkoa alisema kabla ya uzinduzi huo kufanyika yatafanyika makongamano ambayo yatatoa fursa kwavijana kujadili mambo mbalimbali yanayohusu maslahi ya Taifa, ikiwa ni pamoja na uzalendo na namna ambavyo Baba wa Taifa Mwalimu Julias Nyerere alikuwa mfano wa kuigwa kwa uzalendo wake.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment