Na: Mwandishi Wetu, Mbozi
Mkuu wa mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Mstaafu Nicodemus
Mwangela leo amepokea msaada wa Sare za vijana wa Halaiki katika sherehe za
uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 na madawati 120 kwa ajili ya shule
mbili za sekondari vyote vyenye thamani ya zaidi ya Sh.29.8Milioni kutoka Benki
ya NMB.
Akizungumza kwenye hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika
viwanja vya ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Songwe Meneja wa Kanda ya Nyanda za Juu
Kusini Straton Chilongola alisema lengo la Benki yake ni kusaidia maendeleo ya
jamii kupitia Nyanja za elimu na Afya na kwamba benki hiyo imetenga zaidi ya
Sh.1bilioni kwa ajili hiyo.
Alifafanua kuwa benki hiyo imetoa Truck Suit 800 kwa ajili
ya vijana wa halaiki ya Mwenge zenye thamani ya Sh.19,824,000 na msaada wa viti
na meza 120 kwa ajili ya shule za sekondari za Ndugu na Vwawa Day zote zilizopo
katika halmashauri ya wilaya ya Mbozi yenye thamani ya Sh.10milioni na kufanya
msaada huo kuwa na thamani ya Sh.29,824,000.
Akizungumza mara baada ya kupokea vifaa hivyo Mkuu huyo wa
mkoa alisema NMB ni wadau muhimu wa maendeleo ya wananchi na kwamba imekuwa
benki ya mfano kwa utoaji huduma bora kwa wajasiriamali, wakulima kupitia Amcos
na hata kwa mtu mmoja mmjoa.
Alisema michango ya NMB katika kuleta maendeleo imejikita
katika masuala ya msingi ya elimu na afya kwa kuwa wanatambua umuhimu wa elimu
na afya katika jamii na kuwa suala la afya pia ni pamoja na masuala ya michezo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment